• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi apiga Marufuku manunuzi ya vifaa vya rejareja miradi ya madarasa

Posted on: November 11th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi leo tarehe 10 Novemba 2021 amepiga marufuku kwa Halmashauri kununua vifaa vya ujenzi kama vile mbao, nondo, mabati na saruji kwa ajili ya miradi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa kununuliwa rejareja kwa wafanyabiashara badala ya kuagiza kwa pamoja viwandani.

Mheshimiwa Hapi amepiga marufuku hiyo alipokuwa anaendelea na ziara ya siku tatu kukagua miradi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa katika Shule za Sekondari na Shule Shikizi za Msingi katika Wilaya za Rorya, Tarime na Serengeti.

“Mwongozo wa Serikali na Mkoa ni kuwa vifaa vyote vinunuliwe kwa ujumla kutoka viwandani ili fedha hizi ziweze kutosheleza mahitaji katika ujenzi wa vyumba vya madarasa, atakayepindisha tutashughulika nae kabla hatujashughulikiwa sisi” alisema Mheshimiwa Hapi.

Amewataka Wakurugenzi na Watendaji wa Halmashauri kufuata maelekezo yote ya Serikali yaliyotolewa pamoja na fedha hizo na kukamilisha ujenzi wa vyumba vya madarasa hadi kufikia tarehe 1 Desemba 2021.

Mheshimiwa Hapi ameikemea Halmashauri ya Wilaya ya Tarime kwa kuwatumia baadhi ya wakandarasi katika kujenga vyumba vya madarasa ambao wanatuhumiwa katika miradi mingine ambapo suala hilo lipo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) na uchunguzi wake unaendelea.

“Haiwezekani kazi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa mnawapa wazabuni ambao baadhi yao wanatuhumiwa kupewa zabuni katika miradi iliyotelekezwa vibaya katika Halmashauri hii na uchunguzi wake upo TAKUKURU unaendelea” alisema Mheshimiwa Hapi.

Wazabuni waliopewa kazi ya kujenga vyumba hivyo ni pamoja na Dapol Construction (08), Juma Kenan (04), Afiki Mara Investment (05) Jura Tanzania Limited (60) huku mafundi wa kawaida wakipatiwa vyumba 10 na kubakia na vyumba 29 ambavyo bado mafundi wanatafutwa.

Mkuu wa Mkoa amezitaka Halmashauri katumia miradi hii kujenga ofisi za walimu hususan katika shule ambazo zimepatiwa madarasa mengi ili kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia.

Mheshimiwa Hapi akiwa katika Wilaya ya Tarime alikagua ujenzi wa madarasa mawili katika Shule ya Sekondari ya Mogabiri, ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa na ofisi katika Shule Shikizi ya Msingi ya Kedere na  ujenzi wa vyumba vya madarasa vinne katika Shule ya Sekondari ya Ingwe.  

Katika Wilaya ya Serengeti, Mkuu wa Mkoa alikagua ujenzi wa vyumba sita vya madarasa katika Shule ya Sekondari ya Mapinduzi Day na vyumba vya madarasa manne katika Shule ya Sekondari ya Serengeti.

Katika vyumba vya madarasa vinavyojengwa kutokana na fedha za Mpango wa Maendeleo na Mapambano dhidi ya UVIKO 19, Halmashauri ya Mji wa Tarime imepewa vyumba vya madarasa 32, Halmashauri ya Wilaya ya Tarime imepewa vyumba vya madarasa 116 wakati Hamashauri ya Wilaya ya Serengeti imepatiwa vyumba vya madarasa 102. 

Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa aliambatana na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mara Mheshimiwa Samwel Kiboye, Wakuu wa Wilaya za Tarime na Serengeti na baadhi ya wajumbe wa Kamati za Usalama za Wilaya, madiwani na watumishi wa halmashauri.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Dkt. Vincent Mashinji ameeleza kuwa kwa sasa kuna miradi ya vmadarasa katika shule tatu ambayo kazi ya kunyayua ukuta imeshaanza lakini mingine ipo katika hatua ya msingi. 

“Hata hivyo miradi ya ujenzi imepata changamoto baada ya pampu ya maji kuungua katika mradi wa maji wa Manchira na hivyo Mji wa Mugumu kukosa maji ya uhakika na hivyo kukwamisha shughuli za ujenzi kuendelea vizuri” alisema Mheshimiwa Mashinji.

Hata hivyo ameeleza kuwa tayari kifaa kilichoungua kilikuwa kimepatikana na mafundi walikuwa wanaendelea kurekebisha pampu hiyo na maji yalikuwa yanategemea kurejea katika hali ya kawaida muda sio mrefu.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa