• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi aongoza wanamara kumbukumbu ya Mashujaa

Posted on: July 29th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi leo tarehe 25 Julai, 2022 amewaongoza wananchi wa Mkoa wa Mara kufanya usafi, kuomba dua na kutoa heshima ikiwa ni sehemu ya kumbukumbu ya mashujaa.

Kumbukumbu hiyo ilianza saa 12.00 asubuhi kwa kufanya usafi katika Soko la Saa Nane lililopo katika Manispaa ya Musoma ambapo Mheshimiwa Hapi aliwahamasisha wananchi kufanya usafi katika maeneo yao ili kuweza kudhibiti magonjwa yanayotokana na uchafu.

“Magonjwa yanayotokana na uchafu ni mengi na yanatumia gharama kubwa kuyatibu yasipodhibitiwa katika kufanya usafi vizuri katika maeneo tunayoishi” alisema Mheshimiwa Hapi.

Aidha, akiwa katika eneo hilo Mheshimiwa Hapi amezindua rasmi ghuba la kuwekea uchafu na kuiagiza Manispaa ya Musoma kuondoa dampo lisilo rasmi kwenye makazi ya watu katika Soko la Saa Nane na badala yake takataka zitupwe katika ghuba hilo.

Mheshimiwa Hapi pia alitumia fursa hiyo kuwahamasisha wananchi waliojitokeza kufanya usafi kushiriki katika Sensa ya Watu na Makazi kwa mwaka 2022 ambayo itafanyika hapa nchini tarehe 23 Agosti, 2022.

“Sensa hii itaiwezesha Serikali kujua idadi ya watu, mahitaji yao ya msingi na nini kifanyike katika kuwaletea maendeleo wananchi” alisema Mheshimiwa Hapi.

Baada ya usafi, msafara ukaelekea Parokia ya Kanisa Katoliki Rwamlimi ambapo kuna mnara wa kumbukumbu ya ndege ya kivita iliyoanguka katika eneo hilo wakati wa vita vya Kagera.

Katika eneo hilo, kulikuwa na dua kutoka kwa viongozi wa dini, gwaride la heshima pamoja na salamu kutoka kwa viongozi mbalimbali.

Akizungumza katika eneo hilo, Mheshimiwa Hapi amewataka wananchi kuwaenzi mashujaa wa Taifa letu kwa kutenda mazuri waliyokuwa wanayapigania na kudumisha umoja, amani na mshikamano wa Taifa.

Kumbukumbu ya Mashujaa kitaifa ilifanyika Kitaifa katika Mkoa wa Dodoma ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa