• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi akemea mivutano Rorya

Posted on: May 18th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi leo amehudhuria kikao cha Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Rorya na kukemea mivutano inayoendelea katika halmashauri hiyo baina ya madiwani.

Akizungumza katika kikao hicho, Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa amepata taarifa za malumbano ya viongozi na wananchi wa wilaya hiyo tangu wilaya ilipoanza mpaka sasa na matokeo ya malumbano hayo ni kuchelewesha miradi ya maendeleo ya wananchi.

“Mheshimiwa Rais analeta fedha hapa zifanye maendeleo, lakini badala yake fedha zinakuja na hazitumiki kwa sababu mnavutana kila mtu anataka mradi ujengwe katika eneo lake, huku mkiendelea kuwaumiza wananchi” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa Halmashauri hiyo imepokea fedha kuanzia tarehe 25 Februari, 2022 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kata ya Labour, lakini mpaka sasa mradi huo umesimama kwa sababu madiwani wanabishana sehemu ya kujenga kituo hicho.

“Sasa, ninatoa siku saba ujenzi wa Kituo cha Afya Labour uwe umeanza na ninahitaji taarifa ya utekelezaji wa mradi huu”aliagiza Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa anafahamu kikao cha baadhi ya madiwani wa Halmashauri hiyo kilichokaa Sirari katika Wilaya ya Tarime kupanga njama ya kumuondoa madarakani Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mheshimiwa Ng’ong’a Gerald Samweli na viongozi wengine katika wilaya hiyo na kuwataka madiwani hao kuacha mara moja.

Aidha, Mheshimiwa Hapi amewaonya wanamara wanaochochea malumbano yasiyo na tija katika Mkoa wa Mara na kukwamisha miradi ya maendeleo ya wananchi kuacha tabia hiyo.

Mheshimiwa Hapi amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kuhakikisha madeni yote ambayo Halmashauri inadai yanalipwa ili kuiwezesha Halmashauri hiyo kulipa madeni yake ikiwemo madeni ya posho za vikao vya madiwani.

Mheshimiwa Hapi amewaonya madiwani kuacha malumbano mara moja na wakiendelea na malumbano hayo Mkoa utamshauri Mheshimiwa Rais kuvunja Baraza la Madiwani la Halmashauri hiyo kwa mujibu wa Sheria ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.

Akizungumza na wananchi wa vijiji vya Makongorosi na Urio katika Kata ya Labour, Mheshimiwa Hapi amewataka wananchi wa Kata hiyo kushikama ili kufanikisha maendeleo ya Kata hiyo.

Kwa upande wake, Katibu wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mara Bwana Langaeli Akiyoo ameeleza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameleta fedha nyingi za miradi ya maendeleo katika Wilaya ya Rory ana kuwataka madiwani wasimamie utekelezaji wa miradi.

“Ninawaomba msimamie utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa manufaa ya wananchi waliowachagua” alisema Bwana Akyoo.

Bwana Akyoo amewakubusha madiwani kuwa wapo katika Baraza hilo kwa sababu wananchi na vyama vyao viliwaamini watawaletea maendeleo katika eneo hilo, wasiipoteze imani hiyo.

Wakati huo huo, Mkuu wa Wilaya ya Rorya Mheshimiwa Juma Chikoka ameeleza kuwa umoja na mshikamano ni muhimu sana wakati huu ambapo Serikali inaleta fedha za kuijenga Rorya.

Akizungumza wakati wa kikao cha Baraza hilo, Mheshimiwa Chikoka ameemeza kuwa kwa sasa kipaumbele kikubwa kwa Wilaya ya Rorya ni kuinua mapato ya ndani ya Halmashauri hiyo ili yaweze kutekeleza miradi ya maendeleo ya wananchi.

“Mapato yakiimarika Halmashauri itakuwa na uwezo wa kutekeleza miradi ya maendeleo na kutoa mikopo kwa makundi mbalimbali ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kwa mujibu wa Sheria” alisema Mheshimiwa Chikoka.

Mheshimiwa Chikoka ameeleza kuwa kwa sasa Halmashauri inampango wa kuanzisha stendi mpya ya mabasi katika eneo la Mika na shilingi bilioni moja zimetengwa kwa ajili ya kazi hiyo katika bajeti yam waka ujao wa fedha.

Aidha, Mheshimiwa Chikoka ameeleza kuwa Halmashauri pia inaongeza nguvu za uwekezaji katika mazao ya biashara ya pamba, alizeti na kahawa na viongozi wa Wilaya ya Rorya watakuwa na mashamba ya mfano ya mazao haya.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa