• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi akagua maandalizi ya kutekeleza miradi

Posted on: November 5th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ametembelea Wilaya ya Rorya na Tarime kukagua maandalizi ya ujenzi wa miradi ya madarasa na vituo vya afya vilivyotengewa fedha na serikali.

Mheshimiwa Hapi ametembelea maeneo hayo leo tarehe 16 Oktoba 2021 na kutoa maelekezo kwa viongozi kuhusiana na maandalizi hayo.

“Lengo la ziara hiii ni kuangalia maeneo ambapo miradi hii itajengwa pamoja na kukagua maandalizi ya kuanza kwa miradi hii mara baada ya fedha kuruhusiwa kuanza kutumika.

Mheshimiwa Hapi alitembelea mradi wa upanuzi wa zahanati kuwa Kituo cha Afya Nyamagaro na ujenzi wa Madarasa katika Shule ya Sekondari ya Nyamtinga katika Wilaya ya Rorya.

Aidha akiwa katika Wilaya ya Tarime, Mheshimiwa Hapi alitembelea mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya katika eneo la Kitenga katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime na mradi wa ujenzi wa madarasa katika Shule ya Sekondari ya Nkende katika Halmashauri ya Mji wa Tarime. 

Akizungumza na wakati akitembelea miradi hiyo Mheshimiwa Hapi amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kuendelea na maandalizi ya ujenzi huo pamoja na kuunda kamati za ujenzi huo mapema iwezekanavyo.

Aidha Mheshimiwa Hapi amevielekeza vyombo vya ulinzi na usalama kufuatilia miradi hiyo ikiwa ni pamoja na kuwachukulia hatua watu wote watakaohusika na ubadhilifu wa aina yoyote ile katika miradi hiyo.

Mheshimiwa Hapi amemuagiza Meneja wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) kuhakikisha barabara ya kuingia katika Shule ya Sekondari Mtinge inapitika muda wote.

Aidha amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha maeneo ambayo miradi hii inaenda kujenga hayana migorogo na wananchi.

“Serikali haina fedha za kuanza kulipa watu fidia, kama maeneo yaliyoainishwa katika miradi hii yana mgogoro, leteni mapendekezo ya kupeleka miradi hiyo maeneo mengine haraka iwezekanavyo” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi amewataka watendaji wote watakaohusika katika utekelezaji wa miradi hiyo kutimiza wajibu wao kwa wakati ili wananchi waweze kupata huduma za kijamii zinazokusudiwa kutoaka na miradi hiyo.

Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa pia alipata nafasi ya kuzungumza na wananchi wa eneo la Nyamagaro katika Wilaya ya Rorya na maeneo ya Kitenga na Nkende katika Wilaya ya Tarime.

Katika ziara hiyo Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa aliambatana na Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa Wilaya, Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa, Mwakilishi wa Afisa Elimu wa Mkoa, Wenyeviti wa Halmashauri, Wakurugenzi wa Halmashauri na watendaji wengine.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa