• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi aipongeza Manispaa ya Musoma

Posted on: July 12th, 2022

Mkuu wa Mkoa Mheshimiwa Ally Salum Hapi leo tarehe 12 Julai, 2022 ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Musoma kwa kupata hati safi ya ukaguzi kwa hesabu za Mwaka 2020/2021 na kuitaka Halmashauri hiyo kuongeza nguvu katika usimamizi wa mapato na matumizi.

Mheshimiwa Hapi ametoa kauli hiyo wakati alipohudhuria kikao maalum cha Baraza la Madiwani kwa ajili ya kujibu hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) za mwaka 2020/2021.

“Ninawapongeza sana kwa kupata hati safi lakini kutokana na taarifa hii ninataka Halmashauri iendelee kuchukua hatua za kuimarisha usimamizi katika makusanyo ya mapato ya ndani” alisema Mheshimiwa Hapi.

Aidha Mheshimiwa Hapi ameipongeza Manispaa ya Musoma kwa kufanya vizuri katika kusimamia makusanyo ya mapato ya ndani ambapo mpaka sasa Halmashauri hiyo ipo katika asilimia 104.

Mheshimiwa Hapi amemtaka Mkurugenzi wa Manispaa ya Musoma kuhakikisha wakusanya mapato 47 ambao hawajasainiana mkataba na Manispaa hiyo kufanya hivyo haraka iwezekanavyo ili kuondoa uwezekano wa upotevu wa fedha za Halmashauri.

Aidha amemtaka Mkurugenzi kufuatilia suala la baadhi ya wananchi waliolipia lesseni ambao hawakukatiwa lesseni za biashara zao na vibanda vya Halmashauri ambavyo vimepangishwa bila kulipiwa kodi ya vibanda.

Mhehsimiwa Hapi amemuagiza Mkurugenzi wa Manispaa ya Musoma kuimarisha Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani ili kiweze kutimiza majukumu yake kwa mujibu wa sheria na kuisaidia Halmashauri hiyo kubaini changamoto mbalimbali na kuziondoa kabla ya Wakaguzi wa Nje hawajaziandika.

Mheshimiwa Hapi ameitaka Halmashauri hiyo kukarabati magari chakavu ili yaweze kutumika na kufanya utaratibu wa kuyaondoa magari hayo katika vitabu vya Halmashauri.

Ameitaka taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kukamilisha uchunguzi na kupelewa suala la madai ya shilingi milioni 272 za Mkandarasi Norplan TZ Ltd mahakamani na kuvishirikisha vyombo vingine vya dola katika kuwatafuta viongozi wa VIMU Saccoss wanaodaiwa na Manispaa ya Musoma shilingi milioni 48 walizokopeshwa.

Kwa upande wake, Meya wa Manispaa ya Musoma Mheshimiwa William Gumbo ameeleza kuwa Halmashauri itatekeleza maagizo yote ambayo yametolewa na Mkuu wa Mkoa.

Hata hivyo Mstahiki Meya ameeleza kuwa Manispaa hiyo inakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa ardhi ya akiba na hivyo kuwahitaji kulipa fidia katika miradi mbalimbali ya maendeleo inayoanzishwa kutoa huduma kwa wananchi.

Ameeleza kuwa kuhusu mapato kukusanywa kinyume na sheria inatokana na wananchi kugomea kulipia baadhi ya huduma na ushuru kulingana na ilivyopangwa na Halmashauri hiyo na badala yake kulazimisha kulipia pungufu.

Manispaa ya Musoma ilikuwa na hoja 66 za ukaguzi ambamo kati yake kuna hoja za nyuma 22, hoja za mwaka 2020/2021 37 na maagizo 07 ya kikao cha Kamati ya Bunge la Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC). Aidha kati ya hoja hizo, hoja 22 zimefungwa wakati hoja 44 zinaendelea.

Kikao hicho pia kimehudhuriwa Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa, Kamati ya ulinzi ya Wilaya ya Musoma, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), wataalamu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mwakilishi Mkazi wa CAG Mkoa wa Mara na Wakuu wa Vitengo na Idara za Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa