• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi aagiza Maafisa Mipango kuzisaidia Halmashauri

Posted on: July 22nd, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi leo tarehe 18 Julai, 2022 amewakumbusha Wakuu wa Idara za Mipango kuzisaidia Halmashauri katika kufuatilia, kutekeleza na kusimamia vipaumbele vya Halmashauri likiwemo suala la lishe.

Akizungumza katika kikao cha kufanya tathmini ya utekelezaji wa Afua za Lishe katika Mkoa wa Mara kilichofanyika leo katika ukumbi wa Uwekezaji, Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa bila ya Maafisa Mipango kutoa kipaumbele kwenye suala la lishe, utekelezaji wake unaweza kuwa mgumu.

“Mtu wa kuwakumbusha viongozi kuhusu masuala yote muhimu ya Halmashauri ni Mkuu wa Kitengo cha Mipango, akilala huyu Halmashauri yote inalala lakini akitimiza wajibu wake vizuri atawakumbusha viongozi na wahusika kuhusu majukumu muhimu ya Halmashauri ” alisema Mheshimiwa Hapi.

Aidha amewakumbusha Waweka hazina wa Halmashauri kulipa fedha zote zilizoidhinishwa na Wakurugenzi na kama kuna sababu ya kutokulipa Mwekahazina anatakiwa kumpa mrejesho Mkurugenzi au yoyote aliyetoa idhini ya malipo na sio kuamua tu yeye mwenyewe kulipa, kulipa pungufu au kutolipa kabisa.

Mheshimiwa Hapi ameagiza Waweka Hazina wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda na Halmashauri ya Wilaya ya Butiama kuwasilisha maelezo kwa Katibu Tawala wa Mkoa kutokana na kutokulipa kiasi cha fedha kilichoidhinishwa na wakurugenzi wao kwa ajili ya kutekeleza Afua za Lishe.

Aidha amemuagiza Mkurugenzi wa Mji wa Bunda kumpangia majukumu mengine Afisa Lishe wa Halmashauri hiyo ambaye amesababisha Halmashauri kushindwa kutumia fedha zilizokuwa zimepangwa kwa ajili ya Afua za Lishe katika Halmashauri hiyo.

Mheshimiwa Hapi amechukua hatua hizo kutokana na baadhi ya Halmashauri kufanya vibaya katika viashiria vya utekelezaji wa Afua za Lishe kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo Halmashauri kutokutoa kipaumbele katika utekelezaji wa suala la lishe kulingana na miongozo ya Serikali.

Mheshimiwa Hapi amezipongeza Halmashauri zilizofanya vizuri katika suala la kutenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wa Afua za Lishe ikiwa ni pamoja na Manispaa ya Musoma asilimia 98.07, Halmashauri ya Mji wa Tarime asilimia 84.86 na Halmashauri ya Wilaya ya Tarime asilimia 83.12.

Aidha Halmashauri zilizofanya vibaya katika kipengele hicho ni Halmashauri ya Wilaya ya Bunda asilimia 6.64, Halmashauri ya Mji wa Bunda asilimia 26.26 na Halmashauri ya Wilaya ya Butiama asilimia 28.52.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa kuna madhara makubwa kwa serikali wananchi wakiwa hawana lishe bora kwa sababu Serikali inapoteza fedha nyingi kuhudumia wagonjwa ambao asilimia kubwa yanachangiwa na lishe duni.

Kwa upande wake, Afisa Lishe wa Mkoa wa Mara Bwana Paul Makali ameeleza kuwa pamoja na juhudi mbalimbali zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali pamoja na wadau, bado suala la lishe ni muhimu sana kupewa kipaumbele ili kuondokana na madhara ya lishe duni.

Bwana Makali ameeleza kuwa waathirika wakubwa wa lishe duni ni Watoto chini ya umri wa miaka 5 ambao wasipopata lishe bora wapo katika hatari ya kudumaa.

“Kwa sasa Mkoa wa Mara una watoto chini ya miaka mitano wenye udumavu wapatao 132,000 ambao ni wengi na hatimaye Mkoa utakuwa na watu wengi ambao wanaudumavu katika kukua kwao jambo ambalo ni tatizo katika jamii” alisema Bwana Makali.

Bwana Makali amezitaka Halmashauri kuongeza mkazo kwenye utekelezaji wa Afua za Lishe hususan kwenye masuala ambayo hayahitaji fedha kama vile kutoa ushauri nasaha kwa akina mama wanaohudhuria kliniki, kugawa matone ya vitamin A na kadhalika.

Kikao cha tathmini ya Afua za lishe katika Mkoa wa Mara kilihudhuriwa pia na Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Wakuu wa Idara, Vitengo na baadhi ya wataalamu wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Waweka Hazina, Wakuu wa Idara za Mipango, Waganga Wakuu na Maafisa Lishe wa Halmashauri.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa