• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Fox Divers wakabidhi kombe la ushindi kwa RC

Posted on: February 25th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Mtambi leo amempokea ofisini kwake Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mara na Rais wa Klabu ya Timu ya Mpira wa Kikapu ya Fox Divers Mhe. Esther Matiko akiambatana na viongozi wengine wa klabu hiyo waliokuja kukabidhi kombe la ushindi wa timu hiyo katika michuano ya Ligi Kuu ya Tanzania.

Akizungumza baada ya kupokea kikombe hicho, Mhe. Mtambi amempongeza Mhe. Matiko kwa kazi kubwa anayoifanya kuinua vipaji vya vijana na kushughulikia masuala mbalimbali ya kimaendeleo katika Mkoa wa Mara.

“Ninakupongeza sana Mhe. Matiko na taasisi ya Matiko Foundation kwa namna mnavyojitoa kushughulikia masuala mbalimbali ya kimaendeleo katika Mkoa wa Mara” amesema Mhe. Mtambi na kumhakikishia kuwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara inaunga mkono shughuli zote za kimaendeleo bila kujali itikadi za kisiasa.  

Mhe. Mtambi ameipongeza Klabu ya Fox Divers kwa ushindi wao katika Ligi ya Klabu Bingwa ya Mpira wa Kikapu Tanzania na kufuzu kuwania ubingwa wa dunia katika mashindano yatakayofanyika mwaka huu.

Mhe. Mtambi amemuomba Mhe. Matiko kusaidia jitihada za Serikali ya Mkoa za kuwahamasisha wazawa wa Mkoa wa Mara kuchangamkia fursa mbalimbali za uwekezaji zilizopo na kuwekeza katika Mkoa wa Mara ili kukuza uchumi wa Mkoa.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Fox Divers Bwana Aloyce Renatus amesema Klabu hiyo ilipata ushindi katika fainali zilizofanyika katika uwanja wa Chinangali, Mkoani Dodoma tarehe 14 Desemba, 2024.

Bwana Renatus amesema kutokana na ushindi huo Klabu hiyo imefanikiwa kuchaguliwa kuiwakilisha Tanzania katika Mashindano ya Klabu Bingwa Afrika yatakayofanyika katika nchi ya Rwanda kuanzia tarehe 14 Desemba, 2025.

Bwana Renatus amesema kwa sasa timu hiyo inaendelea na maandalizi ya kuwania ubingwa wa Afrika na ikishinda itakuwa imeutangaza Mkoa wa Mara na Tanzania kwa ujumla.   

Kwa upande wake, Mhe. Matiko amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa mapokezi mazuri na ushirikiano anaoupata kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na kumuomba Mhe. Mtambi awe mgeni rasmi tarehe 28 Februari, 2025 katika ufungaji wa mashindano ya Matiko Cup yanayoendelea katika Wilaya ya Tarime.

“Shughuli mbalimbali zitapamba ufungaji huu ikiwemo mashindano ya nyama choma na tunaangalia kama tutaweza kumleta msanii mkubwa aweze kutumbuiza wakati wa shughuli hiyo” amesema Mhe. Matiko.

Hili ni kombe la pili Mhe. Matiko anakabidhi kwa Mkuu wa Mkoa baada ya mwaka 2024 Mhe. Matiko kukabidhi kombe la ushindi la Bunda Queens ambayo yeye alikuwa ni mlezi wake baada ya kushinda katika mashindano kama hayo.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mtambi afungua kambi ya madaktari bingwa na bobezi 64 Mara

    June 23, 2025
  • Watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mara wapatiwa mafunzo

    June 20, 2025
  • Mara mshindi wa pili UMITASHUMTA 2025

    June 18, 2025
  • Zingatieni miongozo ya kilimo cha tumbaku- Dkt. Haule

    June 18, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa