• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

DKT. KIRUSWA: wanaodai fidia walete vielelezo

Posted on: November 7th, 2022

Naibu Waziri wa Madini Mheshimiwa Dkt. Steven Kiruswa amewataka wajumbe wa Nyabigena Mining Society Limited wanaodai fidia baada ya eneo lao la uchimbaji kuchukuliwa na Mgodi wa Dhahabu wa North Mara kuwasilisha vilelelezo vya madai hayo katika Ofisi ya Afisa Madini Mkazi, Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Kiruswa ametoa agizo hilo baada ya kufanya mazungumzo yaliyowahusisha viongozi wa Mkoa wa Mara, Wilaya ya Tarime, wabunge, madiwani na viongozi wa ushirika wa Nyabigena Mining Society Limited tarehe 6 Novemba, 2022 katika ukumbi wa Shule ya Sekondari ya Tarime kujadili mustakabali wa madai hayo.

“Ninatoa hadi tarehe 30 Novemba, 2022 vielelezo na Ushahidi wote uwasilishwe ili uweze kuhakikiwa na Serikali kwa ajili ya kujiridhisha kabla ya wanaodai kulipwa stahiki zao” alisema Dkt. Kiruswa.

Katika kikao hicho pia, Mheshimiwa Kiruswa amemtaka Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Mara kuendelea kutoa elimu kwa wananchi hao na viongozi wa ngazi mbalimbali kuhusu taratibu zilizopo katika kupata haki zao katika madai ya fidia ya ardhi na mali nyingine zilizokuwepo.

Aidha, Dkt. Kiruswa amemtaka Mkurugenzi Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Barrick North Mara Apolinary Lyambiko kuwasilisha nyaraka na vielelezo vinavyoonyesha mikataba kati ya mgodi huo na Vijiji vitano vilivyoingia mkataba na mgodi huo ili kubaini nani alipaswa kuwalipa wananchi hao.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Tarime Kanali Michael Mtenjele amemshukuru Naibu Waziri kwa kuweza kuja na kusikiliza wananchi hao wenye madai ya fidia na kupunguza malalamiko ya wananchi wa Wilaya ya Tarime.

Kwa upande wake Mbunge wa Tarime Vijijini Mheshimiwa Mwita Waitara amewataka viongozi wa makundi ya wanaodai fidia kuungana wao kwa wao na kuwa na kauli moja katika madai yao ili kuweza kurahisisha kusikilizwa na madai yao kupatiwa ufumbuzi.

Mheshimiwa Waitara amewataka walalamikaji kuwasilisha vielelezo vyao halali na kutoa taarifa kwa viongozi na Serikali kuhusu udanganyifu wowote unaoweza kutokea ili wapate haki yao.

Mheshimiwa Waitara amewataka wananchi hao kuwasilisha madai halali na kutoa taarifa zote muhimu ili wananchi wenye haki katika madai hayo waweze kulipwa fidia zao.

Kwa upande wake, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Mara Mhandisi Joseph Kumburu ameeleza kuwa tayari ofisi yake imemteua Afisa atakayepokea taarifa na vielelezo vyote katika Kituo kidogo cha kuuza madini katika eneo la Nyamongo Wilayani Tarime.

“Watu wote wenye madai wanaweza kuwasilisha vielelezo vya madai yao kwenye ofisi hiyo iliyopo Nyamongo kuanzia tarehe 7 Novemba, 2022 ili kuwarahisishia kufika kwa urahisi” alisema Mhandisi Kumburu.  

Wachimbaji wa Nyabiguna Mining Society Limited 362 ndio walikuwa waanzilishi wa uchimbaji wa madini katika eneo hilo ambapo baadaye liliuzwa na vijiji vyao kwa Mgodi wa Dhahabu wa North Mara lakini katika kulipa fidia baadhi yao walilipwa wengine hawakulipwa kabisa.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa