• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

DC aagiza kukamatwa kwa viongozi na wananchi Bukama

Posted on: August 23rd, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mhe. Dkt. Vicent Naano Anney amemuagiza Mtendaji wa Kata ya Nyamuswa na Mtendaji wa Kijiji cha Bukama kuwakamata na kuwafikisha kwenye vyombo vya shheria viongozi wa kijiji cha Bukama na wazazi na walezi wa wanafunzi wa Shule ya Msingi Bushore waliogoma kuchangia chakula cha watoto shuleni.

Mhe. Dkt. Anney ametoa maagizo hayo baada ya kupokea taarifa kutoka kwa Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Mradi wa Project Zawadi na Diwani wa Kata hiyo wakilalamikia kitendo cha wazazi wa wanafunzi wa shule hiyo kugoma kuchangia chakula cha watoto wao kwa madai kuwa wakichangia chakula hicho kitaibiwa na walimu.

“Ninaagiza kuanzia wiki ijayo, chakula kiwe kinatolewa katika shule hii, kama hakipo kamata viongozi wa kijiji na wote wanaokataa kuchangia chakula peleka polisi ili waende mahakamani, haiwezekani tunabembelezana katika masuala ya msingi kama chakula cha watoto shuleni” amesema Mhe. Dkt. Anney.

Mhe. Dkt. Anney amesema kuweka chakula shuleni sio hiari bali ni maelekezo ya Serikali na kuwataka wananchi wa Kijiji cha Bukama kuacha uzembe, uchoyo, roho mbaya na chokochoko zisizo na tija na badala yake kuchangia chakula kinachohitajika ili watoto wao waweze kusoma vizuri na kuweza kubadili matokeo ya shule hiyo.  

Mhe. Anney amepongeza Shirika la Project Zawadi kwa mchango mkubwa wanaoutoa katika kukuza elimu katika Tarafa ya Chamriho, Wilaya ya Bunda kwa kusaidia ujenzi wa miundombinu, mafunzo kwa walimu, mafunzo ya kilimo kwa wanafunzi na wanajamii na ufadhili kwa wanafunzi wanaotoka katika mazingira magumu.

Mhe. Dkt. Anney amemtaka Katibu Tawala wa Wilaya ya Bunda kuhakikisha Shirika hilo linaalikwa kwenye vikao vya tathmini ya Lishe katika Wilaya ya Bunda ili kuhakikisha kuwa shirika hilo linatambulika katika wadau muhimu wa maendeleo katika ngazi ya Wilaya na Mkoa.

Aidha, ameagiza shule zote za Wilaya ya Bunda kutumia maeneo ya shule angalau ekari tatu kwa ajili ya kilimo cha chakula cha wanafunzi ili kuongezea kwenye chakula kinachotolewa na wazazi wa wanafunzi na kuhakikisha shule zote watoto wanakula angalau mara moja kwa siku.

Akiwa katika eneo hilo pia, Mhe. Dkt. Anney amekemea imani za kishirikina kwa wanaopata ugonjwa wa kuharisha na kutapika badala ya kuzingatia kanuni za afya katika makazi yao, na kukemea unyanyasaji wa wanawake na watoto yatima kwa kuwanyanganya mali zao baada ya kufiwa na waume au wazazi wao.

Kwa upande wake, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Busore Victor Magaji Magaji amesema shule hiyo ilijengwa mwaka 1974 na kwa sasa ina wanafunzi 77 wa awali na wanafunzi 381 wa madarasa ya msingi na ina walimu nane na ilikuwa na nyumba tatu za walimu.  

Mwalimu Magaji amesema changamoto kubwa inayoikumba shule hiyo ni wazazi wengi kukataa kuchangia chakula cha wanafunzi kwa kisingizio kuwa wakichanga kitaliwa na walimu wa shule hiyo jambo ambalo linaifanya shule hiyo kupata matokeo yasiyoridhisha.

Mwalimu Magaji amelishukuru Shirika la Project Zawadi kwa kutoa ufadhili kwa wanafunzi wa shule hiyo wanaotoka katika mazingira magumu kwa kuwapatia mahitaji yote muhimu ya shule.  

Katika taarifa yake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Project Zawadi Bi. Regina Mkama ameiomba Serikali kuwahamasisha wananchi kuchangia chakula shuleni ili watoto waweze kupata walau mlo mmoja ili kuboresha ufaulu wa wanafunzi na kuacha kuwatesa watoto kwa njaa wakiwa shuleni.

Bi. Mkama amesema walimu walikubali kuwaachia wawakilishi wa wazazi kusimamia suala la chakula cha wanafunzi lakini bado wazazi hawataki kuchangia ili watoto wale shuleni kama zilivyo katika  shule nyingine za Wilaya ya Bunda.

Bi. Mkama amewashukuru wananchi waliojitolea katika miradi ya maendeleo iliyotekelezwa katika shule hiyo na kuwataka wasikatishwe tamaa na wenzao wanaopinga kushiriki katika miradi ya maendeleo.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa