• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Daraja litakamilika ndani ya wiki tatu: Malima

Posted on: April 13th, 2021

Ujenzi wa daraja la zege katika barabara ya Sirari Mwanza eneo la Nyamsangula wilayani Tarime ambapo kalavati lililokuwepo lililosombwa na maji umeanza na unategemea kukamilika baada ya wiki tatu.

Hayo yameelezwa na Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima wakati akizungumza na wananchi katika eneo hilo leo tarehe 12 Aprili 2021.

“Awali kalavati lililokuwepo lilikuwa na kipenyo cha mita tano lakini sasa daraja linalojengwa litakuwa na vipenyo viwili vya mita tano kila moja ili kupitisha maji mengi zaidi” alisema Mheshimiwa Malima.

Mheshimiwa Malima ameeleza kuwa katika ajali hiyo ambayo ilitokea tarehe 11 Aprili 2021, watu watatu wamefariki dunia na maiti zao zimepatikana baada ya kusombwa na maji yaliyokuwa yamefurika katika eneo hilo.

Mheshimiwa Malima amewapongeza wananchi kwa juhudi zao za kuweka daraja la muda ambalo litasaidia watoto kuvuka kwa ajili ya kwenda shule, hata hivyo ameiagiza TANROADS kuimarisha usalama wa daraja hilo la muda ili kunusuru maisha ya watu watakaokuwa wanavuka hapo.

Aidha Mheshimiwa Malima ameipongeza Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi pamoja na Wakala wa Barabara (TANROADS) kwa jitihada kubwa zilizofanyika ili kurejesha mawasiliano katika barabara hiyo kwa haraka.

Kwa upande wake Kaimu Meneja wa TANROADS ameeleza kuwa ajali hiyo ilisababishwa na mvua kubwa zilizokuwa zinaendelea kunyesha ambazo zilisomba kipande kikubwa cha bati lililoziba maji yaliyokuwa yanapita katika calvati hiyo na kusababisha mafuriko.

Mhandisi huyo ameeleza kuwa kwa sasa magari yote yanayoenda na kutoka Kenya yanapita katikati ya mji wa Tarime wakati daraja hilo linapoendelea kujengwa.

Tayari mkandarasi yupo eneo la tukio na ameanza kazi ya kujenga daraja hilo ikiwa ni pamoja na kuweka daraja la muda ili wananchi waweze kupita.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa