• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Chikoka awataka washiriki wa Miss Lake Zone kutangaza vivutio vya utalii

Posted on: August 19th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Rorya Mhe. Juma Chikoka amemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mara katika mapokezi ya washiriki wa mashindano ya Miss Lake Zone, 2024 na kuwataka washiriki hao kuvitangaza vivutio vya utalii vya Kanda ya Ziwa.

Mhe. Chikoka ametoa wito huo katika mapokezi ya washiriki hao yaliyofanyika katika hoteli ya Le Grand Beach baada ya kuhitimisha ziara ya siku nne ambapo washiriki hao walitembelea vivutio vya utalii vilivyopo katika Mkoa wa Mara.

“Mikoa ya Kanda ya Ziwa ina vivutio vingi vya utalii vinavyotokana na uwepo wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Ziwa Victoria na hifadhi nyingine na vivutio vya asili vya utalii ambavyo Watanzania wanapaswa kuvijua na kuvitembelea” amesema Mhe. Chikoka.

Mhe. Chikoka amesema Watanzania walio wengi wanapaswa kuhamasishwa kufanya utalii wa ndani katika vivutio vilivyopo Kanda ya Ziwa inayounganisha Mikoa ya Mara, Simiyu, Mwanza, Shinyanga, Geita na Kagera.

Aidha, amewapongeza washiriki hao kwa kuutembelea Mkoa wa Mara ambao unamiliki Zaidi ya asilimia 75 ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, sehemu kubwa ya Ziwa Victoria na umebarikiwa kuwa na madini mengi na kuvutia wawekezaji wa madini katika kila Wilaya.  

Mhe. Chikoka amewataka washiriki wote kuzingatia kauli mbiu ya mashindano hayo Urembo na Uongozi kwa kufuata mwenendo mzuri unaozingatia maadili, kujituma na unyenyekevu ili kuweza kufika mbali katika maisha yao.

Amewatolea mfano wa waliokuwa wasanii katika fani mbalimbali ambao kwa sasa ni viongozi mahiri wakutegemewa katika Taifa mfano Jokate Mwongero na Mwana FA ambao kwa sasa wanaweza kuwatumia kama mfano bora wa kuigwa.

“Mimi pia nilitoka kwenye Sanaa lakini kutokana na kazi nzuri, unyenyekevu na maisha niliyoishi, nikateuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Rorya, ninajua hata ninyi mkijitahidi inawezekana” amesema mhe. Chikoka.

Kwa upande wake Meneja wa Le Grand Victoria Hotel Bwana Paul Mutinda amewataka washiriki hao kutumia ubunifu katika kuutangaza utalii wa ndani kwa Watanzania ili kuwavutia watu wengi Zaidi kutembelea vivutio vya utalii.

Bwana Mutinda amesema urembo ni fani inayohitaji ubunifu na kuwataka washiriki hao kuwa wabunifu katika fani hiyo ili kuweza kunufaika na fursa mbalimbali zinazotokana na kushiriki katika tasnia hiyo.

Kwa upande wake, mwandaaji wa mashindano hayo Bi. Rosemary Selemani Range amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Afred Mtambi kwa kuwasaidia washiriki hao kuweza kufanya ziara ya siku nne katika Mkoa wa Mara kutembelea vivutio vya utalii.

Bibi Range ameeleza kuwa fainali za mashindano hayo zinategemewa kufanyika tarehe 31 Agosti, 2024 katika Hoteli ya Malaika Beach iliyopo katika Mkoa wa Mwanza na kuwakaribisha wananchi wa mikoa ya Kanda ya Ziwa na Mikoa jirani kushiriki katika hafla hiyo.

Amesema kama waandaji wa mashindano hayo, watayafanyia kazi maoni ya wadau kuhusiana na mashindano hayo na kuyaboresha Zaidi kadiri siku zinavyoenda.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa