• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

CCM yawataka Watanzania kumuenzi Mwalimu Nyerere kwa vitendo

Posted on: April 24th, 2025

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi leo ameendelea na ziara yake katika Mkoa wa Mara katika Wilaya ya Butiama na kuwataka watanzania kumuenzi Mwalimu Nyerere kwa vitendo.

Akizungumza katika ziara ya miaka 61 ya Muungano wa Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar katika Wilaya ya Butiama, Dkt. Nchimbi amesema katika uhai wake Baba wa Taifa alihamasisha amani, umoja na mshikamano wa kitaifa na kukemea ubaguzi wa aina yoyote ile.

“Baba wa Taifa alipigania sana amani, umoja na mshikamano wa Tanzania na akaeneza lugha ya Kishwahili kwa Watanzania wote ili kuujenga umoja wa Kitaifa, tuendelee kumuenzi kwa vitendo kwa kuunga mkono mazuri yote aliyotuachia” amesema Mhe. Nchimbi.  

Balozi Nchimbi amewataka Watanzania kujihadhari na viongozi wa siasa wanaohamasisha uvunjifu wa amani, ukabila na vurugu na badala yake kutumia uchaguzi unaokuja kuwachagua viongozi bora wanaopenda maendeleo.  

Mhe. Nchimbi amesema miradi aliyoitembelea katika Mkoa wa Mara ya Uwanja wa Ndege Musoma, Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere na Chuo Kikuu cha MJNUAT Butiama ni miradi ya kimkakati na inaenzi maono na matamanio ya Mwalimu Nyerere na Serikali ya awamu ya sita imeitekeleza kwa ufanisi mkubwa.

Mhe. Nchimbi amewataka wanachama wa CCM na wananchi wa Wilaya ya Butiama kushiriki uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, kuhuisha taarifa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na kuhakikisha kuwa kura za CCM ni asilimia 100 ili kumuenzi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini amesema ujenzi wa miradi mikubwa ya kimkakati katika Wilaya ya Butiama imebadilisha sura ya Butiama kimaendeleo.

Mhe. Sagini ameitaja miradi hiyo kuwa ni Chuo Kikuu cha MJNUAT Butiama, Sekondari ya Amali ya Mkoa wa Mara, Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Butiama na Chuo cha VETA, mradi wa maji wa Mgango- Kiabakari- Butiama ambayo imelifanya eneo hilo kuwa eneo na hali tofauti kuliko lilivyokuwa awali.

Mhe. Sagini amemuomba Mhe. Nchimbi kuingiza mradi wa ukarabati wa Daraja la Kirumi lililopo katika Mto Mara katika Ilani ya Uchaguzi ya Mwaka 2025-2030 ili daraja hilo liwekwe katika miradi ya kipaumbele katika utekelezaji wa ilani hiyo.

Katika ziara hiyo, Mhe. Nchimbi ametembelea Kaburi la Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ametembelea na kukagua ukarabati na ujenzi wa Chuo Kikuu cha Mwalimu Julius Kambarage Nyerere cha Kilimo na Teknolojia (MJNUAT) Butiama na kuzungumza na wananchi katika Kampasi kuu ya chuo hicho na kuwasalimia wananchi katika eneo la Kiabakari.

Balozi Nchimbi ameambatana na viongozi na Watendaji wa CCM na Serikali na kauli mbiu ya miaka 61 ya Muungano ni “Muungano wetu ni Dhamana, heshima na tunu ya Taifa, Shiriki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025”. 

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa