• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Bunda yatoa mapendekezo ya Mgawanyo wa Halmashauri

Posted on: April 28th, 2020

Mkuu wa Wilaya ya Bunda Mwalimu Lyidia Bupilipili ameiomba Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMESEMI) inapogawa upya halmashauri za Wilaya ya Bunda kuzingatia suala la upatikanaji wa huduma kiurahisi kwa wananchi.

Mheshimiwa Bupilipili ameeleza hayo leo tarehe 22 Aprili wakati wa ziara ya Katibu Mkuu TAMISEMI Eng. Nyamhanga katika Wilaya ya Bunda.

“Ofisi yangu inapendekeza kuwa Halmashauri ya Mji wa Bunda iwe na Tarafa mbili za Serengeti na Chamliho na Halmashauri ya Wilaya ya Bunda iwe na tarafa mbili za Kenkombyo na Nansimo ili kuwarahisishia wananchi kupata huduma” alisema Mwalimu Bupilipili.

Ameeleza kuwa kwa sasa Wilaya hiyo ina tarafa nne ambapo Halmashauri ya Mji wa Bunda ina tarafa moja wakati Halmashauri ya Wilaya ya Bunda ina tarafa tatu ambapo mbili zipo upande mmoja wakati nyingine ipo upande mwingine wa wilaya na hivyo kuwalazimisha wananchi kuvuka mji wa Bunda ili kwenda kupata huduma ilipohamia Halmashauri ya Wilaya upande mwingine ambako ni mbali.

Mheshimiwa Bupilipili ameeleza kuwa ofisi yake imependekeza kuwa ofisi za makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Bunda yajengwe Kibara kama ilivyopendekezwa na Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo na mapendekezo hayo tayari yamewasilishwa TAMISEMI.

Awali, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda Mwalimu Amos J. Kusaja alisema Halmashauri ilipokea agizo la kuhamishia ofisi zake kwenye maeneo yao ya utawala na Baraza la Madiwani waliamua kuhamishia ofisi katika mji wa Kibara ambako wako hadi sasa.

Bwana Kusaja alisema Baraza la Madiwani liliamua Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ijengwe katika Tarafa ya Chamliho na Menejimenti ya Halmashauri ilipendekeza kuwa kutokana na hilo, ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Bunda zijengwe katika kijiji cha Makongoro jirani na hospitali ya wilaya mapendekezo ambayo hayakupitishwa na Baraza la Madiwani.

“Baada ya maamuzi ya madiwani, sisi katika menejimenti hatuna tena suala lingine tunasubiria maamuzi ya TAMISEMI na viongozi wengine” alisema Bwana Kusaja.

Kwa Upande wake Katibu Mkuu TAMISEMI, Mhandisi Joseph Nyamhanga amesema TAMISEMI hufanya maamuzi yake kutegemea mapendekezo yaliyopokelewa na hususan maamuzi ya Baraza la Madiwani ambayo ni ya kisheria.

“Yaleteni tena mapendekezo hayo tuyaangalie vizuri, ili yaweze kufanyiwa kazi mara moja” alisema Eng. Nyamhanga.

 Katibu Mkuu TAMISEMI alikuwa na ziara ya siku tatu katika Wilaya ya Tarime, Serengeti na Bunda katika Mkoa wa Mara kuanzia tarehe 20 Aprili 2020 hadi tarehe 22 Aprili 2020.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa