• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Biashara United yakabidhiwa kwa Mwekezaji

Posted on: January 13th, 2023

Timu ya Biashara United iliyocheza Ligi Daraja la Kwanza iliyopo Mkoani Mara leo imekabidhiwa kwa mwekezaji mpya Free Sports Limited ili aweze kuiendeleza timu hiyo baada ya viongozi na wanachama Biashara United kushindwa kuiendesha.

Akizungumza baada ya kushuhudia makabidhiano hayo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu ameeleza kuwa makabidhiano hayo yanafungua ukurasa mpya kwa timu hiyo.

Bwana Makungu ameelezea kufurahishwa na makubaliano yaliyofikiwa baina ya Biashara United na mwakilishi wa Free Sports Limited na kuhitimishwa na makabidhiano yaliyofanyika mbele ya viongozi wa Mkoa wa Mara.

“Ni matumaini yangu, wananchi wa Mkoa wa Mara na hususan wapenzi wa soka wataunga mkono makubaliano yaliyofikiwa na kuendelea kuisaidia timu ya Biashara United” amesema Bwana Makungu.

Bwana Makungu ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Michezo ya Mkoa wa Mara ameahidi kutoa ushirikiano kwa Timu hiyo na mwekezaji mpya na kutoa ushauri pale utakapohitajika.

Akizungumza baada ya kukabidhi timu hiyo, Kaimu Mwenyekiti wa Klabu ya Biashara United Bwana Agustine Mgendi ameeleza kuwa wanashukuru sana kupata mwekezaji wa kuendelea na timu hiyo.

“Tumemtafuta mwekezaji kwa muda mrefu, tunashukuru sasa amepatikana na ataiendeleza timu na kutoa fursa kwa vijana na watanzania kwa ujumla kupitia klabu hiyo” amesema Mgendi.

Aidha, Bwana Mgendi ameushukuru uongozi wa Mkoa wa Mara kwa kuratibu makubaliano hayo ikiwa ni pamoja na kushuhudia makabidhiano ya Timu hiyo kwa mwekezaji mpya.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Free Sports Limited Bwana Masau Bwire amesema kuanzia sasa mwekezaji atahakikisha kuwa timu hiyo inafanya vizuri na inapanda daraja ndani ya muda mfupi ili iweze kurudi kwenye Ligi Kuu ya Tanzania.

“Tutahakikisha kuwa ndani ya muda mfupi ujao, Biashara United itaingia Ligi Kuu na kushika nafasi nzuri katika msimamo wa ligi kama ilivyokuwa katika kipindi cha 2021/2022” amesema Bwana Bwire.  

Bwana Bwire amewaomba wananchi wa Mkoa wa Mara kuendelea kuiunga mkono na kuishangilia kwani bado itaendelea kuwepo katika Mkoa wa Mara.

Bwana Bwire ameeleza kuwa awali, Kampuni hiyo ilikuwa inaisaidia timu kulipa gharama mbalimbali ikiwemo mishahara ya wachezaji na benchi la ufundi, usafiri, malazi na chakula.

Aidha, Bwana Bwire ameushukuru sana uongozi wa Mkoa kwa kusimamia makubaliano na kushuhudia makabidhiano ya timu hiyo yanafanyika kwa maridhiano ya pande zote.

Makabidhiano hayo yameshuhudiwa na Kamati ya Usalama ya Mkoa, Menejimenti ya Mkoa wa Mara, wadau wa michezo na viongozi na wawakilishi wa wanachama wa Klabu ya Biashara United.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa