• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Bashungwa awataka wananchi kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Posted on: November 11th, 2024

Waziri wa Ujenzi Mhe. Innocent Bashungwa leo tarehe 10 Novemba, 2024 amezindua ofisi na kuongoza harambee ya ukamilishaji wa ofisi za Jimbo Katoliki Bunda na kuwataka wananchi kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika tarehe 27 Novemba, 2024.

Akizungumza wakati wa harambee hiyo, Mhe. Bashungwa amewataka wananchi kushiriki kikamilifu matukio mbalimbali ya uchaguzi ikiwemo kuhudhuria kamapeni za uchaguzi ili kuwatambua wanaogombea na sera zao kwani ni muhimu kuwajua kabla ya kufanya maamuzi ya kuwachagua viongozi.

“Tumepewa fursa ya kuwachagua viongozi watakaowatumikia kwa kipindi cha miaka mitano ijayo, ninaomba kuwasihi muitumie vuzuri fursa hii na kuwachagua viongozi bora watakaoshirikiana na Serikali kuwaletea maendeleo” amesema Mhe. Bashungwa.

Mhe. Bashungwa amewataka wananchi kushiriki kikamilifu uchaguzi ili wasiwalaumu watu wengine kwa kuwachagulia viongozi watakaowaongoza na kuwataka kutumia vizuri fursa hii na kuwachagua viongozi wazuri na wapenda maendeleo.

Mhe. Bashungwa amemshukuru Askofu Mwasondole kwa kumualika kushiriki katika harambee hiyo ambapo yeye na wafanyakazi wa ofisi yake wameahidi kuchagia shilingi 62,700,000 kwa ajili ya ukamilishaji wa Jimbo Katoliki Bunda.

Mhe. Bashungwa ameeleza kuwa kwa sasa Jimbo Katoliki la Bunda lina miaka 13 tu tangu lilipoanzishwa na limefanikiwa kufanya mambo mengi na ni matumaini yake kuwa litakapofikisha miaka 25 ya jubilee yake litakuwa limepiga hatua kubwa ya maendeleo.

Mhe. Bashungwa amewataka viongozi wa dini kuendelea kuliombea Taifa na kuwaombea viongozi wa Serikali ili Mungu awalinde na awawezeshe kutekeleza majukumu yao kwa manufaa ya Watanzania wote.  

Ametumia fursa hiyo kuelezea miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika Mkoa wa Mara katika Sekta ya Ujenzi ikiwemo miradi ya barabara, madaraja, ukarabati wa uwanja wa undege wa Musoma na mzani wa Robanda, Wilaya ya Bunda unaopima magari yakiwa kwenye mwendo inayotekelezwa na Wakala wa Barabara (TANROADS).

Mhe. Bashungwa ameeleza kuwa Serikali imekarabati vivuko vya MV Musoma na MV Mara na kujenga jengo la abiria katika eneo la Mwigobero, Manispaa ya Musoma na inampango wa kujenga jengo la kupumzikia abiria na kukarabati gati la kupaki vivuko katika eneo la Kinesi, Wilaya ya Rorya. 

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt. Vincent Naano Anney amewataka wananchi wa Bunda kushiriki kampeni za vyama vya siasa katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa ili waweze kuwasikiliza na kuzielewa sera na mipango ya vyama hivyo.

“Vyama vitawanadi wagombea wake ambao wanagombea katika nafasi mbalimbali za uongozi na hivyo niwasihi ndugu zangu tushiriki ili kupata uelewa wa wagombea na vyama vyao ili tuwachague tukiwa tunawaelewa” amesema Mhe. Dkt. Anney.

Aidha, Mhe. Anney ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Bunda amewataka wananchi kushiriki uchaguzi tarehe 27 Novemba, 2024 ili kuweza kuwachagua viongozi bora watakaosimamia maendeleo katika maeneo yao.

“Tukiwachagua viongozi wazuri tutaachana na wale viongozi wababaishaji na wanaouza maeneo ya wananchi” amesema Dkt. Anney na kuongeza kuwa kumekuwa na viongozi wengi wanaochaguliwa na wananchi ambao wamekuwa chanzo cha migogoro katika jamii.

Mhe. Dkt. Anney amewasilisha ahadi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi shilingi milioni 3, Katibu Tawala Mkoa wa Mara shilingi 500,000 na ahadi yake yeye mwenyewe shilingi milioni moja na kuwasilisha ahadi za viongozi, watendaji wa Serikali na watu wengine aliowashirikisha kuhusiana na harambee hiyo.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa harambee hiyo, Askofu wa Jimbo Katoliki la Bunda Simon Chibuga Masondole amemshukuru Waziri Bashungwa kwa kuweza kushiriki katika harambee hiyo na kueleze kuwa litakapokamilika jengo hilo litakuwa ni moja ya vivutio vya Mji wa Bunda.

Mhashamu Askofu ameeleza kuwa mpaka wakati huo tayari Jimbo Katoloki la Bunda lilikuwa limekusanya shilingi 62,700,000 ambazo ni michango ya waumini, parokia mbalimbali, vyama vya kitume na wahisani mbalimbali.

Askofu Masondole ameeleza kuwa katika kufanikisha harambee hiyo, Jimbo Katoliki Bunda liliomba mchango kutokana kwa marafiki mbalimbali ambao wamechangia shilingi 71,800,000 taslimu na ahadi ya shilingi milioni moja. 

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Harambee, Jimbo Katoliki la Bunda Bwana Kulwa Kahabi ameeleza kuwa harambee hiyo ni kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za Jimbo Katoliki la Bunda ambayo ilianza mwaka 2022 na inatarajiwa kuhitimishwa mwaka huu.

Bwana Kahabi ameeleza kuwa mwaka 2022 walifanikiwa kukusanya shilingi milioni 240 ambazo zilitumika katika hatua za awali za ujenzi wa ofisi hizo; awamu ya pili ilikuwa mwaka 2023 ambapo walifanikiwa kukusanya shilingi milioni 130 ambazo zimesaidia katika ujenzi wa jengo hilo na kununua vifaa vya ofisi.

Bwana Kahabi ameeleza kuwa katika harambee ya wakati huu, Kanisa linategemea kukusanya shilingi milioni 350 kwa ajili ya ukamilishaji wa jengo la ofisi hizo ili liweze kutoa huduma kwa waumini, watawa na wageni wanaotembelea Jimbo Katoliki la Bunda.

 Katika harambee hiyo Jimbo Katokili la Bunda limefanikiwa kukusanya shilingi 272,657,150 na kati ya fedha hizo fedha taslimu shilingi 24,000,000; fedha zilizowekwa benki 169,227,650 na ahadi ni shilingi 20,230,000 pamoja na ahadi ya Mhe. Waziri.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa