• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Acheni Tegesha -Mtambi

Posted on: May 25th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ameendelea na ziara yake katika Wilaya ya Serengeti ambapo ametembelea Chuo cha Mamlaka ya Ufundi Stadi (VETA) kinachooendelea kujengwa katika Kata ya Uwanja wa Ndege na kuwataka wananchi wa Mkoa wa Mara kuacha kufanya tegesha inakwamisha maendeleo na kupandisha gharama za mradi wa maendeleo.  

Mhe. Mtambi ametoa kauli hiyo baada ya baadhi ya wakazi wa eneo la Burunga kudai kuwa  maeneo yao yamechukuliwa bila kufuata utaratibu na kujenga Chuo cha VETA na mpango wa Serikali kuhamisha barabara inayopita eneo hilo kupisha ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Mugumu mambo ambayo yamethibitishwa katika kikao hicho kuwa sio kweli.

 “Serikali haitamvumilia mtu yoyote anayekwamisha mradi wa maendeleo kwa ajili ya manufaa yake  binafsi na tutamchukulia hatua mtu yoyote atakayefanya hivyo” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amemwagiza Mkuu wa Wilaya ya Serengeti kufuatilia taarifa kuwa  Wakala wa Barabaraa (TANROADS) Mkoa wa Mara iliwazuia wananchi hao kuendeleza maeneo yao kuanzia mwaka 2010 hadi sasa na tayari wameshafanyiwa tathmini tangu mwaka 2019.  

Kwa upande wake, aliyekuwa Mwenyekiti wa Kijiji hicho Bwana Mateso Moses Kairo amesema awali, eneo hilo lilikuwa la Kijiji cha Burunga ekari 72 na Kijiji kiliamua kulitoa kwa Serikali kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha VETA.

Bwana Kairo amesema kuwa baadaye baada ya mawasiliano na Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti, VETA ilipewa eneo la ekari 42 na ekari 10 walipewa Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo vidogo (SIDO) na eneo lililobakia limekuwa ni mali ya kijij hicho.

Bwana Kairo amesema baada ya Serikali ya Kijiji kuvunjwa na eneo hilo kuingizwa kwenye Mamlaka ya Mji, baadhi ya wananchi wasiokuwa waaminifu walilivamia eneo hilo na kudai ni mali yao na wengine kuwauzia wageni waliokuwa wanatafuta maeneo.

Amesema kuwa wananchi waliovamia eneo hio walifungua kesi kwenye Baraza la Ardhi la Kata na Baraza la Ardhi la Wilaya ambapo wameshindwa lakini bado wakija viongozi maeneo hayo wanadai eneo hilo ni lao, vielelezo vya uhalali wa eneo hilo vipo na ndio vilipelekwa mahakamani.

Awali, wananchi wawili walijitokeza kudai fidia kutokana na maeneo yao kuchukuliwa kupisha mradi WA Chuo cha VETA na ujenzi wa barabara ya Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) jambo ambalo lilikuja kuthibitishwa katika kikao hicho kuwa sio sahihi.

Mkuu wa Mkoa amezungumza na wananchi waliokuwepo eneo la ujenzi wa Chuo cha VETA ambapo alitumia nafasi hiyo kusikiliza kero zao na kuzitolea ufafanuzi.

 Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa aliambatana na baadhi ya Wajumbe wa Kamatiya Usalama ya Mkoa, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Serengeti, Viongozi wa Chama cha Mapinduzi, Mwenyekiti na Menejimenti ya Wilaya ya Serengeti na maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, taasisi na Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa