• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtanda awakaribisha wananchi mapokezi ya Mwenge

Posted on: July 3rd, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda leo amewakaribisha viongozi, watendaji na wananchi wote wa Mkoa wa Mara kushiriki katika mapokezi, mbio na mkesha wa Mwenge wa Uhuru wakati wote utakapokuwa katika Mkoa wa Mara.

Mkuu wa Mkoa amesema hayo leo tarehe 3 Julai, 2023 wakati alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu mapokezi ya Mwenge wa Uhuru katika Mkoa wa Mara yatakayofanyika kesho katika viwanja vya Shule ya Msingi Robanda, Wilaya ya Serengeti.

“Ninawaomba viongozi, watumishi na wananchi wa Mkoa wa Mara kujitokeza kwa wingi katika mapokezi ya Mwenge wa Uhuru lakini pia katika mbio zake na mikesha itakayofanyika katika Halmashauri zote za Mkoa wa Mara kuanzia kesho hadi tarehe 12 Julai, 2023”amesema Mhe. Mtanda.

Mhe. Mtanda ameeleza kuwa Mkoa wa Mara umejiandaa vizuri kuupokea na kuukimbiza Mwenge wa Uhuru kwa kushirikiana na wadau mbalimbali waliojitolea kwa hali na mali.

Mhe. Mtanda amewahakikishia wananchi kuwa katika mapokezi, mbio na mikesha na sehemu zote mwenge utakakopita kutakuwepo na burudani na usalama wa kutosha ili kuwawezesha wananchi kuushangilia Mwenge wa Uhuru kwa amani.

Awali, akizungumza katika kikao cha maandalizi ya kuupokea Mwenge wa Uhuru Mhe. Mtanda amewataka viongozi, wadau na watumishi wote walioalikwa kushiriki mapokezi ya Mwenge wa Uhuru bila kukasa.

Aidha, Mheshimiwa Mtanda ameitaka Kamati ya Maandalizi ya Mwenge wa Uhuru Mkoa wa Mara kutekeleza majukumu yake kama ilivyopanga na kuhakikisha mapokezi ya Mwenge wa Uhuru yanafana na kuwa mfano wa kuigwa.

Mwenge wa Uhuru utakabidhiwa katika Mkoa wa Mara kesho ukitokea Mkoa wa Arusha ambapo utakimbizwa hadi tarehe 12 Julai, 2023 na tarehe 13 Julai, 2023 Mwenge wa Uhuru utakabidhiwa kwa Mkoa wa Mwanza katika eneo la Nansio, Ukerewe.

 Kesho Mwenge wa Uhuru baada ya kupokelewa anza mbio zake kwa kukimbizwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti na mkesha wa Mwenge wa Uhuru utakauwa katika mji wa Mugumu.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa