• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtanda atuma salamu kwa wavuvi haramu Mara

Posted on: November 9th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda leo tarehe 9 Novemba, 2023 amekutana na wadau wa uvuvi katika Mkoa wa Mara na viongozi wa vyama vya wavuvi na kutuma salamu kwa watu wote wanaojihusisha kwa namna moja au nyingine na uvuvi haramu katika Mkoa wa Mara.

Mhe. Mtanda ametoa tahadhari hiyo baada ya kupokea taarifa ya wadau wa Uvuvi Mkoa wa Mara iliyoonyesha uvuvi haramu umeongezeka sana katika Ziwa Victoria hali inayosababisha kukosekana kwa samaki katika ziwa hilo.

“Mkoa wa Mara tumejipanga kudhibiti uvuvi haramu, kwa kuanzia tunakutana na wadau wa uvuvi na kutoa elimu ili baadaye tutakapokukamata usiseme umeonewaa au ulikuwa haujui” amesema Mhe. Mtanda.

Mhe. Mtanda ameeleza kuwa wavuvi haramu wanaweza kuwa wanapata samaki kwa wakati huo lakini wanaharibu kabisa kizazi cha samaki na hivyo kufanya ziwa lisiwe na samaki wa kutosha na mwishoni kutakuwa hamna samaki kabisa.

Amewaomba wavuvi wote kutoa ushirikiano kwa Serikali ili kuwabaini watumishi wa Serikali wasio waaminifu wanaoshirikiana na wavuvi haramu katika kudhibiti kabisa uvuvi haramu katika Mkoa wa Mara

Aidha, Mhe. Mtanda amewataka wavuvi kutoa kero zao zote zinazowakabili ili Serikali iweze kuzifanyia kazi amewaahidi wavuvi hao Mkoa wa Mara utaendelea kuratibu vikao kama hivyo ili kupata suluhisho za changamoto zinazowakabili wavuvi.

Akitoa taarifa ya wavuvi, Mwanyekiti wa Umoja wa Wadau wa Wavuvi Mkoa wa Mara na Kanda ya Ukerewe Bwana Matete M. Mgongo ameeleza kuwa wavuvi wanakabiliwa na kero kubwa tatu kuu ambazo ni uvuvi haramu, uharibifu wa nyavu na wizi na unyang’anyi wa samaki wakiwa ziwani.

“Kero hizi zinatufanya wavuvi wengi tuendelee kuwa maskini pamoja na kwamba tunajitahidi kufanya kazi kwa bidii ili kuweza kujikwamua kimaisha” amesema Bwana Mgongo.

Bwana Mgongo ameeleza kuwa kwa sasa kuna wimbi kubwa la wavuvi haramu waliopo katika Ziwa Victoria jambo ambalo limepunguza idadi ya samaki katika mwambao wa ziwa na hususan upande wa Tanzania na wamechukua hatua mbalimbali lakini hawajapata ufumbuzi wa kudumu.

“ Kwa sasa ili kupata samaki, sisi wavuvi wa Tanzania tunalazimika kwenda kuwahonga walinzi wa nchi jirani ili tuweze kuvua katika nchi hiyo ili kuweza kupata samaki wa uhakika” amesema Bwana Mgongo.

Akizungumzia kuhusu uharibifu wa vyavu ziwani ameeleza kuwa uharibifu huo unafanywa na watu wanaosadikiwa kuwa ni wavuvi wa dagaa wanaotuhumiwa kuharibu nyavu za wavuvi wa Sangara na wameshakaa vikao mara nyingi lakini tatizo hilo bado linaendelea.

Kuhusu unyang’anyi na wizi wa samaki, Bwana Mgongo ameeleza kuwa awali walikuwa wanajua ni watu kutoka nje ya nchi lakini kwa sasa wamebaini baadhi ni watanzania na wengine wameshawahi kukamatwa.

Awali, akitoa taarifa kwa Mkuu wa Mkoa, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu ameeleza kuwa sekta ya uvuvi inamchango mkubwa sana kwa uchumi wa Taifa na mwaka 2022/2023 sekta ya uvuvi katika Mkoa wa Mara iliingiza shilingi 27,530,903,400/=.

“Serikali kupitia Halmashauri mbalimbali ilipata shilingi 1,42,910,472 kutokana na ushuru wa maegesho, ushuru wa samaki na ada ya leseni “ ameeleza Bwana Makungu.

Bwana Makungu ameeleza kuwa Mkoa wa Mara una eneo la maji lenye ukubwa wa kilometa za mraba 10,854 na ni shughuli kubwa ya kiuchumi kwa wananchi wanaoishi katika mwambao mwa Ziwa Victoria na una mialo ya uvuvi 127 ambapo kati yake 88 tu ndio inayofanyakazi kwa sasa.

Takwimu zinaonyesha kuwa watu wapatao milioni 4.5 hapa nchini wameajiriwa katika mnyororo mzima wa uvuvi na kwa Mkoa wa Mara wananchi 379,707 wameajiriwa katika mnyororo wa sekta ya uvuvi kutoka katika  Wilaya zinazopakana na Ziwa Victoria za Butiama, Bunda, Musoma na Rorya.

Kikao Mkuu wa Mkoa na wadau wa uvuvi  Mkoa wa Mara ni mwendelezo wa vikao vya Mkuu wa Mkoa na wadau mbalimbali katika kutatua kero zinazowakabili wananchi wa Mkoa wa Mara.   

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa