• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MAANDALIZI YA MAPOKEZI YA MWENGE YAMEKAMILIKA

Posted on: July 3rd, 2023

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu leo ametoa taarifa ya maandalizi ya mapokezi na mbio za Mwenge wa Uhuru katika kikao cha maandalizi ya Mwenge wa Uhuru Mkoa wa Mara na kuwahakikishia wajumbe kuwa maandalizi yamekamilika.

Bwana Makungu ameeleza kuwa ukiwa katika Mkoa wa Mara Mwenge wa Uhuru utakagua, kuzindua na kutembelea miradi ya maendeleo 63 yenye thamani ya shilingi 17,258,727,862.80

“Miradi hii 63 iko katika halmashauri zote tisa za Mkoa wa Mara na kugharimiwa na michango ya wananchi, Halmashauri, Serikali Kuu na wahisani wa maendeleo” amesema Bwana Makungu.

Bwana Makungu ameeleza kuwa miradi ya maendeleo itakayopitiwa na Mwenge wa Uhuru itatoka Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti (7), Halmashauri ya Wilaya ya Butiama (6), Halmashauri ya Wilaya ya Tarime (7), Halmashauri ya Mji wa Tarime (6) Halmashauri ya Wilaya ya Rorya (8) na Manispaa ya Musoma (7).

Kwa mujibu wa Bwana Makungu miradi mingine inatoka katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma (7), Halmashauri ya Mji wa Bunda (8) na Halmashauri ya Wilaya ya Bunda (7).

Kwa upande wake Mratibu wa Mbio za Mwenge, Mkoa wa Mara Bwana Fidel Baragaye imeeleza kuwa Mwenge wa Uhuru utapokelewa katika viwanja vya Shule ya Msingi Robanda, katika Kijiji cha Robanda, Kata ya Ikoma katika Hifadhi ya Jamii ya Ikona (Ikona WMA) iliyopo jirani na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti tarehe 4 Julai, 2023.

Bwana Baragaye ameeleza kuwa katika Mkoa wa Mara Mwenge wa Uhuru utakagua,kuzindua, kutembelea na kuweka mawe ya msingi katika miradi ya afya, elimu, maji, barabara, madaraja, vikundi vya uzalishaji mali vya vijana na kufanya mikutano ya kuwaelimisha wananchi.

“Miradi itakayopitiwa na Mwenge wa Uhuru imegharimiwa na michango ya wananchi 2,212,111,700/=, fedha za Halmashauri 1,351, 300,345/=,  fedha kutoka Serikali Kuu 9,747,566,042,80/= na fedha kutoka kwa wahisani wa maendeleo ni 4,000,714,175/=” amesema Bwana Baragaye.

Bwana Baragaye ameeleza kuwa baada ya mapokezi, kesho Mwenge wa Uhuru utakimbizwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Seregeti, tarehe 5 Julai, 2023 Mwenge wa Uhuru utakimbizwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Butiama, tarehe 6 Julai, 2023 Mwenge wa Uhuru utakimbizwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime na tarehe 7 Julai, 2023 Mwenge wa Uhuru utakimbizwa katika Halmashauri ya Mji wa Tarime.

Mwenge wa Uhuru utakimbizwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Rorya tarehe 8 Julai, 2023, tarehe 9 Julai, 2023 Mwenge wa Uhuru utakimbizwa katika Manispaa ya Musoma, tarehe 10 Julai, 2023 Mwenge wa Uhuru utakimbizwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, tarehe 11 Julai, 2023 Mwenge wa Uhuru utakimbizwa katika Halmashauri ya Mji wa Bunda na hatimaye tarehe 12 Julai, 2023 Mwenge wa Uhuru utakimbizwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.

Bwana Baragaye ameeleza kuwa baada ya kuhitimisha mbio zake katika Mkoa wa Mara, Mwenge utakabidhiwa katika Mkoa wa Mwanza tarehe 13 Julai, 2023 katika eneo la Nansio, Ukerewe.

Kauli mbiu ya Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2023 ni “Tunza Mazingira, Okoa vyanzo vya Maji kwa Ustawi wa Viumbe Hai na Uchumi wa Taifa”.

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda anategemea kuwaongoza viongozi, wakimbiza mwenge, watendaji na wananchi wa Mkoa wa Mara katika mapokezi na makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru. 

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa