• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

HAPI apokea taarifa ya uchunguzi wa matumizi ya fedha za CSR

Posted on: April 20th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi leo amepokea taarifa ya Kamati ya Uchunguzi wa matumizi ya fedha zinazotolewa na migodi kwa ajili ya Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) katika Mkoa wa Mara katika kipindi cha mwaka 2018/2019.

Akipokea taarifa hiyo, Mkuu wa Mkoa amevunja iliyokuwa Kamati ya Maendeleo ya Jamii  (CDC) ambayo iliundwa kinyume cha Sheria na miongozo kuhusiana na usimamizi wa fedha za umma ikisimamiwa na kamati iliyowashirikisha wawakilishi wa Mgodi wa North Mara na wananchi wa vijiji 11 vinavyouzunguka Mgodi wa Dhahabu wa North Mara.

“CDC ilikuwa inatumika kama kichaka cha kupitisha miradi ya fedha za CSR ambazo kimsingi ni fedha za umma, kinyume cha sheria na taratibu za Serikali na bila kuwahusisha wataalamu wa Serikali waliopo katika Halmashauri na Wilaya ya Tarime” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi amemuagiza Meneja Mkuu wa Mgodi wa dhahabu wa North Mara Bwana Apolinary Lyambiko kufanya mabadiliko ya Meneja Uhusiano wa Mgodi huo Bwana Gilbert Mworia ambaye alikuwa Katibu wa CDC ili kupisha uchunguzi wa tuhuma mbalimbali zinazomkabili.

Mkuu wa Mkoa amemuagiza Kamanda wa Kipolisi wa Kanda Maalum ya Tarime- Rorya kufungua majalada maalum ya uchunguzi kwa viongozi wote wa CDC ikiwemo kuhoji walipata wapi mamlaka ya kuunda kamati ya kushughulikia fedha za umma kinyume cha sheria na taratibu za fedha za umma.  

Aidha, Mheshimiwa Hapi amewaagiza Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri zote kuhakikisha migodi yote ya madini iliyopo katika Mkoa wa Mara ambayo haijafanya makubaliano na Halmashauri zinafanya makubaliano hayo ndani ya muda wa mwezi mmoja.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa wa Mara ametoa maamuzi ya serikali kuhusiana na taarifa hiyo kuwa fedha zote za CSR kuwa ni fedha za umma na fedha hizo ni sehemu ya vyanzo vya mapato ya Halmashauri; miradi yote ya fedha za CSR itaibuliwa kuzingatia masuala muhimu ya uibuaji wa miradi ya serikali; uibuaji wa miradi ya CSR upite katika mfumo wa kawaida kuanzia ngazi za vijiji hadi Mkoa; na wataalamu wa Halmashauri washiriki katika kupanga hadi utekelezaji wa miradi hii.

Maamuzi mengine ni kuendelea kutumika kwa mfumo wa Force account katika miradi ya CSR; ushirikishwaji wa wananchi wanaozunguka mgodi katika utekelezaji wa miradi; ukokotoaji wa mapato ya migodi uwe shirikishi kwa wadau wote; manunuzi ya vifaa kuzingatia mahitaji ya mradi; fedha zote za mradi ziwekwe kwenye vijiji mradi unapotekelezwa; muda wa utekelezaji wa miradi kuzingatiwa.

Maamuzi mengine ni wajibu wa kusimamia miradi yote ya CSR ni wa Serikali kupitia Halmashauri na Migodi itapewa taarifa;miradi yote ya CSR kuwa ni mali ya Serikali; mafaili yote ya miradi hiyo yawepo katika eneo la mradi husika; na miradi hiyo iandaliwe upya katika mfumo wa kawaida wa Serikali na kuhusisha wataalamu.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati hiyo ya Uchunguzi Bwana Anselm Mwampoma ameeleza kuwa lengo la uchunguzi huo lilikuwa ni kubaini namna ambavyo rasilimali ya madini yaliyopo katika Mkoa wa Mara yanavyotumika katika miradi ya maendeleo katika Mkoa wa Mara.

Bwana Mwampoma ameeleza kuwa Mgodi wa Dhahabu wa North Mara ulikuwa umetoa jumla ya shilingi 5,750,000,000 katika kipindi hicho cha miaka mitano na kati ya fedha hizo Halmashauri ya Wilaya ya Tarime ilipokea shilingi bilioni 5.2 huku Halmashauri ya Mji wa Tarime ilipokea milioni 510.

Aidha, taarifa hiyo ilieleza kuwa katika mwaka wa fedha 2020/2021 Mgodi ulikuwa umetenga kwenye bajeti Dola za Kimarekani 1.8 milioni kwa ajili ya CSR fedha ambazo bajeti yake ilipitishwa na CDC na kupita katika vikao mbalimbali hadi zilipozuiliwa kutumika na Serikali ya Mkoa wa Mara.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa migodi mingine ya inayofanyakazi zake katika Mkoa wa Mara ikiwemo MMG Gold Mine, Cata Mine, ZEM (T) LTD, pamoja na wachimbaji wadogo haikuwa imeanza kutoa fedha za CSR katika Halmashauri za Wilaya iliyopo kwa mujibu wa Sheria.

Kamati ya kuchunguza fedha za CSR katika Mkoa wa Mara iliundwa na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhandisi Gabriel Robert Luhumbi ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.

Wajumbe wa kamati ya uchunguzi walikuwa Bwana Anselm Mwampoma kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Marehemu Raphael Ndimbo, Usalama wa Taifa, Bwana Ramadhani S. Nkunya kutoka ofisi za TAKUKURU (M), Byalugaba C. Byalugaba kutoka Ofisi ya Madini (M) na Bwana Samson William kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Mapokezi ya taarifa hiyo yamehudhuriwa na Wajumbe wa Kamati ya Siasa (CCM) ya Mkoa wa Mara Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Wakuu wa Baadhi ya Taasisi, wenyeviti wa halmashauri, Kamati ya Usalama ya Mkoa, viongozi wa dini, wamiliki wa migodi na wachimbaji wadogo.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa