• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yang'ara matokeo ya kidato cha sita

Posted on: July 21st, 2023

Mkoa wa Mara umepata ufaulu wa asilimia 100 katika matokeo ya mtihani wa Taifa wa kidato cha sita kwa mwaka 2023 yaliyotangazwa na Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA) hivi karibuni.

Akizungumza katika kikao cha Menejimenti ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kaimu Katibu Tawala sehemu ya Elimu na Ufundi Bwana Makwasa Bulenga ameeleza kuwa kwa mwaka 2023 Mkoa wa Mara umeongeza ufaulu kwa asilimia 0.9 kutoka ufaulu wa asilimia 99.1 wa mwaka 2022.

“Kati ya wanafunzi wote 3091 waliofanya mtihani katika Shule za Sekondari 28, wanafunzi 3090 wamepata daraja la kwanza hadi la tatu na mwanafunzi mmoja tu amepata daraja la nne na hivyo wote wamefaulu” amesema Bwana Bulenga.

Bwana Bulenga ameeleza kuwa katika Shule ya Sekondari ya Bunda wanafunzi 121 walipata daraja la kwanza ambao ni asilimia 95 ya wanafunzi wote 126 waliofanya mtihani katika shule hiyo na kufanikiwa kupata GPA ya 1.7143 na kushika nafasi ya kwanza katika Mkoa wa Mara.

Aidha, Bwana Bulenga ameeleza kuwa kwa mujibu wa matokeo hayo, Shule za Sekondari ya Bunda na Natta zimefanya vizuri na kufanikiwa kuingia kwenye kumi bora kitaifa katika makundi yao.

Bwana Bulenga ameeleza kuwa Shule ya Sekondari ya Tarime imeongoza Kitaifa kwa kuwa na wanafunzi wengi waliopata ufaulu wa daraja la kwanza ambapo jumla ya watahiniwa 357 walipata daraja la kwanza kati ya wanafunzi 498 waliofanya mtihani katika shule hiyo.

 “Katika Shule za Sekondari za Natta, Songe na Buturi wanafunzi wake wote waliofanya mtihani huo wamepata daraja la kwanza na la pili tu” amesema Bwana Bulenga.

Akifafanua kuhusu watahiniwa hao, Bwana Bulenga ameeleza kuwa asilimia 55 ya watahiniwa hao walichaguliwa kujiunga na kidato cha tano mwaka 2021 wakiwa na ufaulu wa daraja la tatu na katika matokeo ya kidato cha sita wamepata daraja la kwanza na la pili.

Bwana Bulenga ameeleza kuwa ufaulu huo ni matokeo ya mkakati maalum wa Mkoa wa Mara wa kutokomeza daraja la nne na sifuri katika ufaulu wa mitihani ya Taifa.  

Bwana Bulenga ameeleza kuwa katika Shule ya Sekondari ya Bunda wanafunzi 121 walipata daraja la kwanza ambao ni asilimia 95 ya wanafunzi wote 126 waliofanya mtihani huo na kufanikiwa kupata GPA ya 1.7143 na kushika nafasi ya kwanza katika Mkoa wa Mara.

Kwa upande wake, Menejimenti ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara imeipongeza Sehemu ya Elimu na Ufundi, Halmashauri, Walimu na wanafunzi waliofanya mtihani huo kwa jitihada zao zilizowezesha kupata matokeo mazuri katika mtihani huo.

Aidha, Menejimenti imeitaka Sehemu ya Elimu na Ufundi kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo ya elimu katika Mkoa wa Mara kuendeleza ufaulu huo kwenye matokeo ya mitihani ya Taifa ya shule ya msingi, kidato cha pili na cha nne.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Rorya wahimizwa kutumia nishati safi ya kupikia

    August 19, 2025
  • Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa awasha Mwenge wa Mwitongo kwa mara ya 61

    August 18, 2025
  • Mwenge wakagua miradi ya bilioni 6 Musoma

    August 18, 2025
  • Maambukizi ya UKIMWI katika Wilaya ya Bunda yamepungua

    August 16, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa