• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara kutoa kinga tiba kwa watoto

Posted on: November 17th, 2023

RC AFUNGUA KIKAO KAZI CHA URAGHABISHI  

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda leo amefungua kikao kazi cha uraghabishi kuhusu zoezi la utoaji wa kinga tiba za magonjwa ya kichocho na minyoo ya tumbo kwa watoto wenye umri wa miaka 5-14 katika Mkoa wa Mara kilichofanyika katika ukumbi wa uwekezaji.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Mtanda amesema zoezi la utoaji wa kinga tiba kwa watoto litafanyika tarehe 23-24 Novemba, 2023 katika Mkoa wa Mara na kuwahakikishia wananchi kuwa kinga tiba hizo ni salama kwa matumizi ya binadamu.

“Mimi nitazindua rasmi zoezi la utoaji wa kinga tiba kwa watoto tarehe 23 Novemba, 2023 katika Shule moja ya Manispaa ya Musoma, niwaombe wazazi kuwaruhusu watoto kupata dawa na kuhakikisha watoto wanakula kabla ya kupewa dawa hizi” amesema Mhe. Mtanda.

Aidha, Mhe. Mtanda amewataka wananchi wote wa Mkoa wa Mara na hususan wanaoishi kando kando ya Ziwa Victoria kuzingatia kanuni za afya ikiwa ni pamoja na kutumia vyoo na maji safi na salama katika matumizi yao ya kila siku.

“Hizi Wilaya ambazo zimetajwa kuwa na magonjwa mengi yanayotokana na kichocho na minyoo tumbo pia zinaongoza kwa kutokuwa na vyoo bora jambo ambalo linaendeleza kuchafua mazingira yao na kuwafanya watoto wa maeneo hayo kuwa hatarini kupata magonjwa” amesema Mhe. Mtanda.

Mhe. Mtanda ametoa wito kwa wananchi kuhakikisha kuwa kwa siku mbili hizo ambapo dawa kinga zitatolewa, watoto wapewe chakula kabla ya kupewa dawa ili kuzuia athari zinazoweza kujitokeza baada ya kumeza dawa hizo.

Mhe. Mtanda amewataka wataalamu wa Afya na Elimu kusimamia vizuri zoezi hilo ili Mkoa wa Mara uweze kuwafikia walengwa kwa asilimia zaidi ya 100.

Akitoa taarifa za zoezi hilo, Bibi Esther Muya Mratibu wa Magonjwa yasiyopewa Kipaumbele katika Mkoa wa Mara ameeleza kuwa zoezi hilo linatarajiwa kufanyika tarehe 23-24 katika shule zote za Mkoa wa Mara na kuwahusisha watoto wenye umri wa miaka 5-14.

Bibi Muya ameeleza kuwa japokuwa magonjwa haya hayapewi kipaumbele, lakini yanaathari kubwa katika jamii ikiwa ni pamoja na kusababisha ulemavu wa muda mrefu, kuathirika makuzi na maendeleo ya mtoto, kuharibika kwa mimba, kupunguza uwezo wa kufanya kazi , hivyo kuleta umasikini kwa mtu binafsi, jamii, na nchi nzima.

Bibi Muya amezitaka athari nyingine kuwa ni pamoja na utapiamlo kwa watoto, upungufu wa damu mwilini, udhaifu unaoweza kukaribisha maradhi mengineyo, presha ya ini, kansa ya kibofu cha mkojo, kuacha shule na upofu.

Ameeleza kuwa kwa ujumla magonjwa ambayo hayapewi kipaumbele ni 17 lakini kwa  Mkoa wa Mara  na Kanda ya Ziwa kwa ujumla magonjw aya minyoo ya tumbo na kichocho yalikuwa hayapewi kipaumbele, yameongeza ulemavu kwa watu na kushindwa kufaya shughuli zao.

Bibi Muya ameeleza kuwa kwa kiasi kikubwa magonjwa haya yanatokana na wananchi kujisaidia katika au jirani na vyanzo vya maji na ndio maana takwimu zinaonyesha Wilaya zilizoathirika zaidi katika Mkoa wa Mara ni Rorya, Musoma na Bunda ambazo zipo kando ya Ziwa Victoria.

 Kikao kazi hicho kilihudhuriwa pia na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Dominucus Lusasi Mwakilishi wa Wizara ya Afya na Mwakilishi wa Ofisi ya Rais, TAMISEMI na baadhi ya maafisa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa