• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi ataka mkakati wa mapato Rorya

Posted on: August 16th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Rorya kuwa na mkakati ambao utaisaidia halmashauri hiyo kuibua vyanzo vipya vya mapato na kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya halmashauri.

Mheshimiwa Hapi ametoa agizo hilo leo tarehe 14 Agosti 2021 wakati alipokuwa katika ziara ya kukagua miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Rorya.

“Mkakati wa mapato ya halmashauri uuangaliwe upya ili kuona kama kuna vyanzo vipya vya mapato na kuimarisha ukusanyaji katika vyanzo vya zamani” alisema Mheshimiwa Hapi.

Aidha ameitaka Halmashauri kukusanya kikamilifu kutoka kwenye vyanzo vyote vya mapato vya halmashauri ili kuweza kuboresha huduma za jamii katika halmashauri hiyo.

Mheshimiwa Hapi ameitaka Halmashauri pia kuwekeza kwenye baadhi ya shughuli za wananchi kama vile kilimo au biashara ambavyo vinategemea kuleta mapato ya halmashauri hapo baadaye.

“Mnaweza kuamua kusimamia wananchi wapate ushauri wa kulima mazao ya biashara au chakula ambayo mnajua wakipata kwa wingi yakiuzwa, halmashauri itapata mapato kutokana na kilimo hicho” alisema Mheshimiwa Hapi.

Ameishauri Halmashauri kuwashirikisha watendaji wa Kata na Vijiji pamoja na Maafisa Tarafa katika zoezi la kuibua vyanzo vipya vya mapato ili kuona uwezekano wa kupanua zaidi uwigo wa vyanzo hivyo na kupokea ushauri wa watendaji hao katika ukusanyaji wa mapato.

Mheshimiwa Hapi amesistiza usimamizi wa matumizi wa mashine za kukusanyia mapato (POSS) zifanyekazi muda wote na mapato yakishakusanywa yaende benki yasitumike kabla ya kuingizwa benki.

Aidha ameitaka Halmashauri hiyo kudhibiti matumizi ya fedha za serikali katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayowagusa wananchi moja kwa moja.

Mheshimiwa Hapi amewataka watendaji wa Kata na Maafisa Tarafa kusimamia usomaji wa mapato na matumizi ya vijiji kwa wananchi wa vijiji husika ili kupunguza malalamiko ya wananchi kwa serikali yao.

Akizungumza kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Rorya Mheshimiwa Juma Chikoka ameeleza kuwa katika Wilaya ya Rorya anavyovipaunmbele ambavyo atavisimamia kwa juhudi na maarifa.

Mheshimiwa Chikoka amevitaja vipaumbele hivyo kuwa ni pamoja kuimarisha  ukusanyanji wa mapato ya Halmashauri ya Rorya kwa kulinda vyanzo vya mapato vilivyopo na kubuni vyanzo vipya vya mapato.

“Ninauhakika ukusanyaji wa mapato ya halmashauri ukiimarishwa, mambo mengine mengi yatakuwa rahisi kufanikiwa hivyo kuongeza huduma za jamii kwa wananchi wa Wilaya ya Rorya” alisema Mheshimiwa Chikoka.

Katika ziara hiyo Mheshimiwa Hapi alikagua miradi ya maendeleo, kuzungumza na wananchi na kuzungumza na viongozi na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa