• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Aweso Mgeni Rasmi Mara Day 2021

Posted on: September 10th, 2021

Waziri wa Maji Mheshimiwa Jumaa Hamidu Aweso (Mb.) anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika kilele cha maadhimisho ya 10 ya Siku ya Mara yatakayofanyika kuanzia tarehe 13 hadi 15 Septemba, 2021 katika Wilaya ya Tarime.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Albert Gabriel Msovela ameeleza hayo leo tarehe 10 Septemba 2021 wakati akizungumza na waandishi wa Habari katika Ukumbi wa Uwekezaji uliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

“Maadhimisho ya mwaka huu yataambatana na shughuli mbalimbali ikiwemo uzinduzi wa Kampeni ya Mkoa ya upandaji Miti kwa kila halmashauri; upandaji wa miti 10,000 na uwekaji wa vigingi 60 katika mipaka ya Bonde la Mto Mara katika vijiji vya Mrito na Kerende vilivyopo Wilayani Tarime” alisema Bwana Msovela.

Bwana Msovela ameeleza kuwa shughuli nyingine zitakazofanyika katika maadhimisho ya mwaka huu ni maonyesho ya wajasiriamali kutoka taasisi mbalimbali za umma na kijamii yatakayoanza tarehe 13 Septemba 2021 hadi tarehe 15 Septemba 2021 katika viwanja vya Chuo cha Ualimu Tarime.

Aidha maadhimisho hayo yatapambwa na michezo mbalimbali inayolenga kuhamasisha jamii kutunza na kuhifadhi vyanzo vya Bonde la Mto Mara kama vile kukimbiza kuku, mpira wa miguu, kukimbia kwenye magunia na kuvuta Kamba.

“Kauli mbiu ya maadhimisho ya Siku ya Mara kwa mwaka 2021 ni Tuhifadhi Mto Mara kwa Utalii na Uchumi Endelevu” alisema Bwana Msovela.

Bwana Msovela ameeleza kuwa Maadhimisho ya Siku ya Mara ni utekelezaji wa maazimio ya Mkutano wa kumi (10) wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Bonde la Ziwa Victoria uliofanyika tarehe 04 Mei, 2012 katika mji wa Kigali nchini Rwanda ambao ulielekeza kufanyika kwa Maadhimisho ya Siku ya Mara (Mara Day) kila mwaka tarehe 15 Septemba kuanzia mwaka 2012.

Bwana Msovela amewaalika wananchi wa Mkoa wa Mara, wafanyakazi, wajasiriamali, na wadau wote wa maendeleo ndani nan je ya Mkoa wa Mara kushiriki kwenye maadhimisho hayo yatakayofanyika katika viwanja vya Chuo cha Ualimu Tarime.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa