• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Wananchi Rorya wahimizwa kutumia nishati safi ya kupikia

Posted on: August 19th, 2025

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Ndugu Ismail Ali Ussi amewahimiza wananchi wa Wilaya ya Rorya kutumia nishati safi ya kupikia katika maeneo yao kutokana na faida mbalimbali zinazopatikana kwa kutumia nishati safi.

Akizungumza na wananchi katika Shule ya Sekondari Nyamunga, baada ya kutembelea mradi wa nishati safi wa shule hiyo, Ndugu Ussi amesema kwa kupikia nishati safi wananchi watapika kwa gharama nafuu na pia watakuwa wanatunza mazingira.

“Nishati safi inasaidia sana kwani gharama zake ni nafuu, haiathiri afya ya mtumiaji kama ilivyo katika matumizi ya kuni na mkaa na inasaidia kutunza mazingira yanayotuzunguka, hivyo ni muhimu sisi sote kutumia nishati safi majumbani mwetu” amesema Ndugu Ussi.

Ndugu Ussi ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Rorya kwa kuwekeza fedha shilingi milioni 11 kwa ajili ya kutekeleza mradi huo katika Shule ya Sekondari Nyamunga ambao amesema unalinda afya za wapishi na mazingira ya Halmashauri hiyo na kuwataka wananchi kuiga mfano huo kuboresha maisha yao.

Wakati huo huo, Mwenge wa Uhuru umeendelea na mbio zake katika Mkoa wa Mara ambapo leo tarehe 19 Agosti, 2025 umeingia katika Wilaya ya Rorya na kutembelea, kukagua, kuweka jiwe la msingi na kuzindua miradi saba ya maendeleo yenye thamani ya shilingi 2,531,470,759.63.

Fedha zilizogharimia miradi hiyo zimetokana na mchango wa wananchi shilingi 6,920,000; fedha za Halmashauri shilingi 184,876,550; Serikali Kuu shilingi 2,286,594,209.63 katika sekta za mazingira, huduma za kiuchumi, mifugo, elimu, maendeleo ya jamii, miundombinu na afya.

Mwenge umepokelewa katika Stendi ya Kinesi kutoka Wilaya ya Butiama na baadaye kuelekea Nyamunga Sekondari ambapo umeweka jiwe la msingi kwenye mradi wa maji Nyamunga na kukagua mradi wa nishati safi, kukagua klabu ya kuzuia na kupambana na rushwa katika Shule ya Sekondari Nyamunga.

Aidha, Mwenge wa Uhuru umetembelea skimu ya umwagiliaji ya Rabour, umeweka jiwe la msingi katika uzio wa mnada Nyamaguku, kuweka jiwe la msingi katika Sekondari ya Jafari Chege, kutembelea gereji ya pikipiki ya kikundi cha vijana wazalendo katika eneo la Utegi.

Katika Wilaya ya Rorya, Mwenge wa Uhuru umezindua daraja la mto Mabura na kalavati mbili za barabara ya Ryagoro-Saro, umeweka jiwe la msingi katika zahanati ya Randa na baadaye kuelekea katika mkesha katika uwanja wa Osogo eneo la Utegi.

Katika eneo la mkesha, Mwenge umepokea Risala ya Utii na kukagua halaiki, kupokea taarifa mbalimbali kuhusiana na maandalizi ya uchaguzi mkuu, masuala ya afya, lishe na kuzuia madawa ya kulevya na rushwa.

Kesho tarehe 20 Agosti, 2025 Mwenge wa Uhuru utaendelea na mbio zake katika Mkoa wa Mara ambapo utakimbizwa katika Halmashauri ya Mji wa Tarime na mapokezi ya Mwenge yanatarajiwa kufanyika katika uwanja wa Shule ya Msingi Gamasara.  

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Rorya wahimizwa kutumia nishati safi ya kupikia

    August 19, 2025
  • Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa awasha Mwenge wa Mwitongo kwa mara ya 61

    August 18, 2025
  • Mwenge wakagua miradi ya bilioni 6 Musoma

    August 18, 2025
  • Maambukizi ya UKIMWI katika Wilaya ya Bunda yamepungua

    August 16, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa