• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Tarime yadhibiti watu kutoka nje kujiandikisha Tanzania

Posted on: September 9th, 2024

Serikali Mkoa wa Mara imedhibiti watu wasio Watanzania kujiandikisha au kuboresha taarifa zao kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa kuwaelimisha wadau wa uchaguzi kusaidia katika udhibiti wa watu wasio raia na kuwasambaza maafisa uhamiaji katika vituo vya kujiandikishia.

Hayo yameelezwa na Mkuu wa Wilaya ya Tarime Meja Edward Gowele alipokutana na waandishi wa Habari ofisini kwake leo tarehe 7 Septemba, 2024 na kueleza kuwa Serikali inahakikisha wanaohusika tu ndio wanajiandikisha au kuboresha taarifa zao.

“Elimu imewasaidia wadau na hususan vyama vya siasa kujua kuwa ni jukumu lao kudhibiti watu kutoka nje ya Tanzania kujiandikisha maana watakuja kupiga kura na kuharibu uchaguzi wetu” amesema Meja Gowele.

Mhe. Gowele amesema zoezi la uandikishaji kwa Wilaya ya Tarime linaendelea vizuri mpaka sasa na mwitikio wa wananchi na hususan vijana wanaojiandikisha kwa mara ya kwanza ni mkubwa na katika baadhi ya vituo imelazimu kuongeza mashine na watumishi wanaohusika na uandikishaji.

Meja Gowele amesema Wilaya ya Tarime imeweka mikakati ya pamoja na Halmashauri zake mbili kuhusu namna ya kulikamilisha zoezi hili na kuwashirikisha wazee wa kimila, viongozi wa dini na viongozi wa vyama vya siasa.

Aidha, amesema Halmashauri zote mbili zimefanya matangazo ya kutosha kuhamasisha wananchi kushiriki na viongozi wa Serikali pia wamekuwa wakipita kwa wananchi kuwahamasisha ikiwemo na kwenye misiba.

Meja Gowele amewahamasisha wananchi wa Wilaya ya Tarime kutumia muda uliobakia kujitokeza na kuboresha taarifa zao katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ambapo kwa Mkoa wa Mara mwisho wa zoezi hilo ni tarehe 10 Septemba, 2024.

Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Sirari Mhe. Amosi Sagala Nyabikwi amesema amewahamasisha mawakala waliowekwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) kudhibiti watu ambao sio watanzania kuboresha taarifa zao au kujiandikisha kuwa wapiga kura.

Mhe. Nyabikwi amesema Wenyeviti wa Vitongoji na wenyeviti wa Vijiji wamesaidia sana katika kuwabaini watu ambao sio wenyeji wa Tarime kwa kusikiliza wanavyoongea, kama hamna mtu anayemfahamu katika kitongoji husika na kwa kuangalia mambo mengine muhimu yanayowatofautisha Watanzania na watu wengine.

Kwa upande wake, Bwana Frank Marwa Yohana amesema vijana wengi wamehamasika na wanajitokeza kujiandikisha au kuboresha taarifa zao wakati huu kutokana na hamasa inayoendelea.

Bwana Yohana amesema vituo vingi vina foleni za watu wanaohitaji kujiandikisha na kuiomba Serikali kuongeza mashine na watumishi katika vituo ili wananchi wasitumie muda mrefu katika vituo vya kuboreshea taarifa zao.

Kwa upande wake, Wakala wa CCM katika kituo cha Sokoni, Sirari Bwana Mbassa Paulo Sasi amesema kuwa kituo hicho kipo jirani na mpaka ambapo raia kutoka nchi za jirani wamekuwa wanataka kuandikishwa kupiga kura Tanzania.

“Kwa sasa vigezo vingine vyote mtu akiwa navyo, tunaangalia chanjo ya ndui, Watanzania tunachanjwa kwenye bega lakini majirani zetu wanachanjwa kwenye mkono sio begani na kwa kutumia njia hii tunawakamata kiurahisi” amesema Bwana Sasi.

 Bwana Mbassa amesema watu wanaokamatwa kwa njia hiyo wanakabidhiwa kwa Jeshi la Uhamiaji ambao wanapita vituoni mara kwa mara kwa ajili ya taratibu za kisheria.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa