• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Serikali yatoa vifaa vya Maabara kwa Sekondari 1258 nchini

Posted on: April 27th, 2020

Serikali imetoa vifaa vya maabara vya masomo ya Kemia, Fisikia na Biolojia kwa shule za sekondari 1258 hapa nchini vyenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni tano ili kuinua kiwango cha elimu hususani masomo ya sayansi hapa nchini.

Akizungumza leo tarehe 20 Aprili 2020 wakati wa kukagua vifaa vya maabara vilivyoletwa katika Shule ya Sekondari ya Kebogwe iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhandisi Joseph Nyamhanga amesema tayari vifaa hivyo vimeshasambazwa na kuanza kutumika katika shule mbalimbali hapa nchini.

“Huu ni uwekezaji mkubwa sana kwa serikali katika sekta ya elimu, na lengo ni kuinua ufundishaji wa masomo ya sayansi kwa wanafunzi wa sekondari hapa nchini” alisema Eng. Nyamhanga.

Eng. Nyamhanga ameeleza kuwa katika bajeti ya mwaka 2020/2021 iliyopitishwa na Bunge hivi karibuni, TAMISEMI imepanga kutoa fedha za ujenzi wa maabara saba za sayansi kwa kila halmashauri hapa nchini ili kuendeleza jitihada za kuinua ufundishaji wa masomo ya sayansi. 

Wakati huo huo, Eng. Nyamhanga ameahidi kuwa TAMISEMI itatoa fedha za kukamilisha ujenzi wa Jengo la Utawala na nyumba ya walimu katika Shule ya Sekondari ya Kebogwe.

Akizungumza baada ya kukagua shule hiyo na kupokea taarifa ya shule, Eng. Nyamhanga amesema “serikali itaunga mkono juhudi za wananchi ambao wamejenga majengo hayo na wameshindwa kuyamalizia”.

Aidha ameipongeza shule hiyo kwa kuendelea kuboresha taaluma ingawa bado ina changamoto ni nyingi ikiwemo za miundombinu ya kujifunzia na kufundishia na nyumba za walimu.  

Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa Sekondari ya Kebogwe ameeleza kuwa shule hiyo ilianza mwaka 2015 kwa kujengwa kwa nguvu za wananchi. Mpaka wakati huu shule ina jumla ya wanafunzi 333 wa kidato cha kwanza hadi cha nne.

 Ameeleza kuwa idadi ya wanafunzi imekua ikiongezeka mwaka hadi mwaka. Shule ilianza ikiwa na wanafunzi 37 wa kidato cha Kwanza lakini mpaka sasa, shule ina wanafunzi 104 wa kidato cha kwanza kwa mwaka 2020.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Rorya wahimizwa kutumia nishati safi ya kupikia

    August 19, 2025
  • Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa awasha Mwenge wa Mwitongo kwa mara ya 61

    August 18, 2025
  • Mwenge wakagua miradi ya bilioni 6 Musoma

    August 18, 2025
  • Maambukizi ya UKIMWI katika Wilaya ya Bunda yamepungua

    August 16, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa