• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Serikali kuwapatia vijana maeneo ya uchimbaji Tarime

Posted on: May 31st, 2024

Serikali imepanga kutenga maeneo ya uchimbaji na kuwagawia vijana wa eneo la Nyamongo, Wilaya ya Tarime ili waweze kujitafutia kipato cha halali kama sehemu ya kukabiliana na uvamizi wa mara kwa mara wa Mgodi wa Dhahabu wa Barrick North Mara.

Waziri wa Madini Mhe. Antony Mavunde amesema hayo wakati wa ziara yake na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhandisi Hamad Masauni katika mkutano wa hadhara na wananchi wanaouzunguka mgodi huo uliofanyika katika uwanja wa Shule ya Msingi Nyabigena, eneo la Nyamongo, Wilaya ya Tarime.

“Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan hataki kuona vijana wakiendeleza kuhangaika na kujihusisha na uvamizi mgodini na ameamua kuwapa maeneo ya uchimbaji na Serikali itawasaidia kuanza kuchimba ili kuwasaidia kutimiza malengo yao katika maisha” amesema Mhe. Mavunde.

Mhe. Mavunde ameeleza kuwa Wizara ya Madini imeweka mkakati wa kuyatumia maeneo ambayo leseni za uchimbaji wa madini zimefutwa kuwapatia vijana ili waweze kujiendeleza katika uchimbaji wa madini na kukuza kipato chao.

Mhe. Mavunde ameliagiza Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) kupeleka mitambo ya kuchoronga madini katika eneo la Nyamongo litakalotengwa kwa ajili ya vijana ili kuongeza tija kwenye uchimbaji katika eneo hilo.

Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhandisi Hamad Masauni amekemea vijana kuvamia mgodi huo na kuliagiza Jeshi la Polisi kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu masuala ya amani na usalama katika maeneo yao.

Aidha, Mhe. Masauni amesema Serikali haifurahii kuona wananchi wanafariki wanapovamia mgodi huo na kulitaka Jeshi la Polisi kuendelea kuimarisha Polisi Jamii katika eneo hilo na kuwachukulia hatua wananchi watakaokamatwa wakivamia mgodi na kuvunja mtandao wa uhalifu unaovamia mgodi huo.

Mhe. Masauni amewataka askari wa Jeshi la Polisi kufanya kazi kwa mujibu wa sheria na taratibu na kumpongeza Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi wa Tarime/Rorya kwa kuwachukulia hatua askari sita ambao wamehusika na matukio ya kutokufuata misingi ya kisheria katika kutekeleza majukumu yao eneo hilo.

Mhe. Masauni amewataka wananchi wa eneo la Nyamongo kufuata sheria za nchi na kuacha kuvamia mgodi na kuwashambulia askari wanapokuwa wanatekeleza majukumu yao katika ulinzi wa mgodi huo, wanannchi na mali zao.

Katika Mkutano huo wananchi wa eneo hilo pia walipewa nafasi ya kutoa maoni, kero na changamoto zinazowakabili na Serikali kutoa majibu ya hoja hizo isipokuwa iliyohusu mgawanyo wa fedha za CSR  kwa sababu suala hilo lipo mahakamani.  

 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Mhandisi Hamad Masauni na Waziri wa Madini Mhe. Antony Mavunde wamefanya ziara Mkoa wa Mara katika Wilaya ya Tarime kuelekea katika mgogoro kati ya wananchi na Mgodi wa Dhahabu wa Barrick North Mara.

Kabla ya kukutana na kufanya mkutano wa hadhara na wananchi, Mawaziri hao walifanya kikao na Kamati ya Usalama ya Mkoa katika ukumbi wa uwekezaji Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na Kamati ya Usalama Wilaya ya Tarime katika Mji wa Tarime.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC azitaka Wilaya kuongeza nguvu maandalizi ya Mwenge 2025

    May 09, 2025
  • Mtambi akabidhi tuzo na kinyago washindi wa Mwenge 2024

    May 09, 2025
  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa