• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Serikali Itaendelea kumuenzi Mhandisi Nyamohanga

Posted on: April 16th, 2025

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko leo tarehe 16 Aprili, 2025 amewaongoza waombolezaji katika mazishi ya aliyekuwa Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mhandisi Boniphace Gissima Nyamohanga yaliyofanyika katika eneo la Mikungani, Wilaya ya Bunda.

Akizungumza katika mazishi hayo, Mhe. Biteko amesema Mhandisi Nyamohanga alikuwa ni hazina kubwa ya mipango inayopimika ndani ya Serikali na amefanya kazi kubwa ndani ya TANESCO, REA na Wizara ya Nishati kwa ujumla.

Mhe. Biteko amesema kazi kubwa alizozifanya kuwa ni pamoja na ukamilishaji wa mradi wa Bwawa la kuzalisha umeme la Nyerere na uanzishaji na utekelezaji wa mpango wa Tanzania kuanza kuuza umeme katika nchi ya Zambia.  

“Sahihi yake aliyoiweka wakati wa kufunga mkataba kati ya Tanzania na Zambia itaendelea kuwepo katika mkataba huo muda wote kutukumbusha Kazi kubwa aliyoifanya Mhandisi Nyamohanga katika sekta ya Nishati” amesema Mhe. Biteko.

Naibu Waziri Mkuu amesema wakati Mhandisi Nyamohanga anateuliwa Shirika lilikuwa lipo katika wakati mgumu sana na kelele za umeme zilikuwa nyingi hapa nchini lakini ametatua tatizo la umeme na kujenga umoja na mshikamano baina ya watumishi wa TANESCO.  

Mhe. Biteko amesema Mhandisi Nyamohanga alikuwa anawatetea na kuwapenda watumishi wake na wakati wote likitokea tatizo alikuwa anasema “wape muda watajirekebisha” amesema Mhe. Biteko na kuongeza kuwa marehemu alikuwa tayari kubeba lawama mbalimbali ili kuwasaidia watumishi wake.

Mhe. Biteko ametumia fursa hiyo kuwaasa waombolezaji wakiwemo viongozi na watendaji kuwa katika maisha yao waige mfano wa Mhandisi Nyamohanga na kuwa baraka ya kuwasaidia wengine na sio kuwa kama kitunguu kusababisha vilio kwa watu wanaomzunguka.

Mhe. Biteko amewataka wanafamilia ya Mhandisi Nyamohanga pamoja na wajane wawili wa marehemu kushikamana, kupendana na kuishi kwa umoja na amani kama wakati ambapo marehemu alipokuwa hai ili waweze kuendeleza maono ya marehemu katika maisha yao.  

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mara Kanali Evans Alfred Mtambi amesema Mhandisi Nyamohanga alikuwa ni mdau muhimu sana katika Maendeleo ya Mkoa wa Mara na amekuwa akitoa ushirikiano mkubwa kwa viongozi wa Mkoa wa Mara.

“Mhandisi Nyamohanga amefariki akiwa njiani pamoja na mambo mengine alikuwa anakuja kukagua na kuona namna ya kupeleka umeme katika Shule ya Amali ya Mkoa wa Mara inayoendelea kujengwa katika Wilaya ya Butiama” amesema Mhe. Mtambi.

Akizungumza katika mazishi hayo, Mhe. Mtambi ameliagiza Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara na Mkoa wa Kipolisi wa Tarime Rorya kuongeza operesheni na watu wote wanaokiuka taratibu za usalama barabarani wachukuliwe hatua za kisheria.

Aidha, Mhe. Mtambi amewataka viongozi, watumishi na wananchi kuiga mfano wa Mhandisi Nyamohanga kwa kuchapa kazi kwa bidii na kutatua kero za wananchi.  

Kwa upande wake, Msemaji wa Familia ya Nyamohanga ambaye pia ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) Mhe. Mwita Gachuma ameishukuru Serikali kwa uratibu mzuri wa mazishi ya Mhandisi Nyamohanga tangu msiba huo ulipotokea tarehe 13 Aprili, 2025

Mhe. Gachuma ameiomba Serikali kusaidia kujenga jengo kwa ajili ya kumkumbuka Mhandisi Nyamohanga katika eneo hilo alipozikwa.

Kwa upande wake, Mbunge wa Musoma Vijijini Prof. Sospiter Muhongo ambaye aliwahi kufanya nae kazi amesema Mhandisi Nyamohanga ni mmoja wa waanzilishi wa bei ya umeme ya 27,000 inayotumika hapa nchini kwa ajili ya kuunganishia umeme wa gharama nafuu na kuiwezesha Tanzania kuingia katika mradi wa Kimataifa wa Power Africa.

Prof. Muhonga ameiomba Serikali kumuenzi Mhandisi Nyamohanga na kutambuliwa kama mwanzilishi wakati wa tathmini ya mradi wa Power Africa itakayofanyika Juni, 2025 ili kukumbuka mchango wake mkubwa alioutoa katika Sekta ya Nishati.

Mhandisi Nyamohanga na dereva wake Ndugu Mujahir Mohamed Haule walifariki katika ajali iliyotokea usiku wa kuamkia tarehe 13 Aprili, 2025 katika Kata ya Nyatwali, jirani na geti kuu la Hifadhi ya Taifa ya Serengeti lililopo eneo la Ndabaka, Wilaya ya Bunda na dereva wake alizikwa tarehe 14 Aprili, 2025 katika Mkoa wa Pwani.

Marehemu Nyamohanga alizaliwa mwaka 1969 na amefariki akiwa na umri wa miaka 56 na kuacha wajane wawili na watoto 15 na wajukuu watano na katika uhai wake alisomea Uhandisi na baadaye  kujiendeleza katika fani za Sheria na Usimamizi wa Biashara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Tumieni magari haya kutatua kero za wananchi- Mtambi

    May 22, 2025
  • CCM yapongeza utekelezaji wa ilani ya uchaguzi Mara

    May 20, 2025
  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa