• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC Nawanda Mgeni Rasmi NANENANE Kanda ya Ziwa Mashariki

Posted on: August 7th, 2022

RC SIMIYU MGENI RASMI NANENANE KANDA YA ZIWA MASHARIKI

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mheshimiwa Dokta Yahya Nawanda kesho anatarajia kuwa mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho ya sikukuu ya wakulima (NANENANE) Kanda ya Ziwa Mashariki katika viwanja vya Nyakabidi, Bariadi Mkoa wa Simiyu.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Kamati ya Maandalizi ya maadhimisho hayo, shughuli katika uwanja wa maonyesho zitaanza saa mbili kamili asubuhi kwa wageni waalikwa kuanza kuwasili katika viwanja vya Nyakabindi.

Ratiba hiyo inaonyesha kuwa Mheshimiwa Nawanda akiambatana na wakuu wa mikoa wa Kanda ya Ziwa Mashariki na viongozi wengine, atatembelea mabanda ya maonyesho kuanzia saa 6.20 na baadaye kuwahutubia wananchi wa Kanda ya Ziwa Mashariki katika viwanja vya Nyakabindi.

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mzee kesho atakagua mabanda ya Halmashauri zote za Mkoa wa Mara kabla ya Mgeni Rasmi kupita katika mabanda hayo.

Ratiba iliyotolewa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mheshimiwa Mzee atakagua mabanda hayo kuanzia saa tatu na nusu asubuhi akiambatana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara na Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mara.

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu leo amekagua mabanda ya maonyesho ya Halmashauri zote tisa za Mkoa wa Mara.

Akiwa katika mabanda hayo, Katibu Tawala aliambatana na baadhi ya Wakuu wa Idara na Vitengo wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara pamoja na viongozi wa Halmashari za Mkoa wa Mara.

Mikoa mitatu inayounda Kanda ya Ziwa Mashariki ni Mara, Shinyanga na Simiyu ambao ndio mwenyeji wa maadhimisho hayo yanayofanyika katika eneo la Nyakabidi, wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu.  

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Rorya wahimizwa kutumia nishati safi ya kupikia

    August 19, 2025
  • Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa awasha Mwenge wa Mwitongo kwa mara ya 61

    August 18, 2025
  • Mwenge wakagua miradi ya bilioni 6 Musoma

    August 18, 2025
  • Maambukizi ya UKIMWI katika Wilaya ya Bunda yamepungua

    August 16, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa