• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC Mtanda aipokea LAAC Musoma

Posted on: March 24th, 2024

Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) leo imetembelea Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara kwa ajili ya kujitambulisha na kusaini kitabu cha wageni na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda katika ukumbi wa uwekezaji uliopo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Akizungumza baada ya kupokelewa Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Stanslaus Mabula ameupongeza Mkoa wa Mara kwa mapokezi mazuri tangu Kamati hiyo ilipowasili tarehe 20 Machi, 2024 katika Wilaya ya Tarime mpaka sasa.

“Kwa niaba ya Kamati, ninaomba kuchukua fursa hii kuwapongeza kwa utekelezaji mzuri wa miradi ya maendeleo tuliyoitembelea na kukagua, miradi yote imesimamiwa vizuri, hongereni sana” amesema Mhe. Mabula.

Aidha, Mhe. Mabula amemshukuru Meya wa Manispaa ya Musoma Mhe. William Gumbo kwa mapokezi mazuri katika Manispaa ya Musoma tangu Kamati hiyo ilipowasili jana.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Said Mohamed Mtanda ameikaribisha Kamati ya LAAC na kuihakikishia kuwa miradi yote inayotekelezwa katika Mkoa wa Mara ipo katika viwango vya ubora vinavyotakiwa na Mkoa umekua ukiwachukulia hatua wale wote wanaojihusisha na matumizi mabaya ya fedha za umma.

“Kwa Mkoa wa Mara hatucheki na wahalifu na tumekua tukichukua hatua kwa wale wote waliotumia fedha za umma kinyume na utaratibu na tuna kesi mbalimbali zilizofunguliwa kwa watu wanaotuhumiwa kufuja fedha za umma” amesema Mhe. Mtanda.

Mhe. Mtanda ametoa mfano wa watumishi na wananchi walioiba mifuko 1,200 ya cementi katika mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mkoa wa Mara ambao kwa sasa wameshafikishwa mahakamani.

Akizungumza katika mapokezi hayo, Mhe. Mtanda ameeleza kuwa kwa sasa Mkoa wa Mara unachangia pato la taifa kwa shilingi bilioni 130-140 kwa mwaka kutokana na shughuli za uchimbaji wa madini katika mgodi mkubwa mmoja na migodi ya kati minne na wachimbaji wadogo zaidi ya elfu kumi waliopo katika Wilaya zote za Mkoa wa Mara.

Mhe. Mtanda ameyataja mapato mengine kutoka Mkoa wa Mara yanatokana na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, ambayo ni asilimia 36 ya eneo lote la Mkoa wa Mara, ambayo kwa mwaka huliingizia taifa mapato ya shilingi bilioni 138 kupitia utalii wa wageni kutoka ndani na nje ya nchi ya Tanzania.  

Aidha, Mhe. Mtanda amesema Mkoa pia umezungukwa na Ziwa Victoria ambapo asilimia 36 za eneo la Mkoa wa Mara ni Ziwa Victoria na Wilaya nne kati ya Wilaya sita za Mkoa wa Mara zinapakana na Ziwa Victoria na hivyo kuufanya uchumi wa Mkoa na hususan wananchi wake kutegemea pia shughuli za uvuvi katika mito na Ziwa Victoria.

Mhe. Mtanda ameeleza kuwa mbali na shughuli hizo, wananchi wa Mkoa wa Mara pia ni wafugaji na wakulima wazuri na hivyo uchumi wa wananchi wengi hutegemea shughuli za kilimo na ufugaji.

Mapokezi hayo yamehudhuriwa pia na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Meya wa Manispaa ya Musoma, Maafisa kutoka Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Wizara ya Fedha, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na Manispaa ya Musoma.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa