• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC awataka washiriki kutumia mafunzo huduma kwa wananchi

Posted on: December 16th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo ameongoza mafunzo kuhusu Uraia na Utawala Bora kwa Kamati ya Usalama ya Mkoa, Kamati ya Usalama ya Wilaya ya Musoma na Menejimenti ya Sektretarieti ya Mkoa wa Mara na kuwataka washiriki kushiriki kikamilifu mafunzo hayo na kutumia elimu watakayopata kuboresha huduma kwa wananchi.

Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo hayo, Mhe. Mtambi amewataka viongozi walioshiriki  mafunzo hayo kufuatilia mafunzo hayo na kuuliza maswali kwa wataalamu hao ili kuboresha utoaji wa huduma na utatuzi wa kero za  wananchi wa Mkoa wa Mara.

“Mafunzo ni muhimu sana katika utekelezaji wa majukumu yetu na yanatukumbusha namna ya kuzingatia Sheria, Kanuni na taratibu tunapotoa huduma kwa wananchi na kutatua kero zinazowakabili wananchi” amesema Mhe. Mtambi.  

Aidha, Mhe. Mtambi ametumia fursa hiyo kuwakumbusha washiriki wa mafunzo hayo kuwatendea haki wananchi kwa kutimiza wajibu wao kikamilifu na kuwasaidia kutatua kero zinazowakabili katika maeneo yao.

Mhe. Mtambi amezishukuru Wizara za Katiba na Sheria, Ofisi ya Rais TAMISEMI na Wizara ya Mambo ya Ndani kwa kuwezesha mafunzo hayo muhimu kwa viongozi na watendaji mbalimbali wa Mkoa wa Mara ambayo yatawasaidia katika utekelezaji wa majukumu yao.  

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Gerald Musabila Kusaya ameishukuru Wizara ya Katiba na Sheria kwa kuandaa, kuratibu na kuendesha mafunzo hayo kwa Kamati za Usalama za Mkoa, Wilaya, viongozi na Watendaji wa Halmashauri zote za Mkoa wa Mara.

Bwana Kusaya amesema mafunzo hayo yatawasaidia watumishi kuboresha huduma na utatuzi wa kero na changamoto za wananchi na kuiomba Wizara ya Katiba na Sheria kutoa mafunzo hayo mara kwa mara kwa makundi mbalimbali ili kuyafanya mafunzo hayo kuongeza tija. 

“Mafunzo ya aina hii yanapaswa kuletwa mara kwa mara ili viongozi na watendaji wengi zaidi waweze kufikiwa na kupatiwa mafunzo haya ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi” amesema Bwana Kusaya.

Akitoa mada katika mafunzo hayo, Bwana Nicolaus Mhagama kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Polisi amewataka washiriki wa mafunzo hayo kutumia elimu waliyoipata katika mafunzo hayo kuwaelimisha wananchi kuhusu mambo mbalimbali ya kitaifa yanayofanywa na Serikali.

Bwana Mhagama amewataka viongozi hao kuwaelimisha wananchi kuhusu taratibu za kisheria, kanuni na taratibu za kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili na hususan namna ya kufanya mashauri yanapokuwa yamefikishwa mahakamani. 

Bwana Mhagama amewataka viongozi kusimamia uadilifu wa watendaji waliopo chini yao na hususan katika ngazi za Kata, Mitaa, Vijiji na Vitongoji ambao wanawahudumia wananchi katika utendaji wao wa kila siku ili kuwafanya wananchi kuongeza imani kwa Serikali yao.

Mafunzo hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Uwekezaji ni sehemu ya Kampeni ya Msaada wa Kisheria wa Mama Samia iliyozinduliwa tarehe 11 Desemba, 2024 na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini katika Uwanja wa Mukendo, Manispaa ya Musoma.  

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Rorya wahimizwa kutumia nishati safi ya kupikia

    August 19, 2025
  • Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa awasha Mwenge wa Mwitongo kwa mara ya 61

    August 18, 2025
  • Mwenge wakagua miradi ya bilioni 6 Musoma

    August 18, 2025
  • Maambukizi ya UKIMWI katika Wilaya ya Bunda yamepungua

    August 16, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa