• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RC awaomba Viongozi wa Dini kukemea maovu

Posted on: May 27th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amekutana na kuzungumza na Kamati ya Amani na Maridhiano ya Mkoa wa Mara katika Ukumbi wa Uwekezaji na kuwaomba viongozi wa dini kukemea maovu katika jamii.

Akizungumza katika kikao hicho, Mkuu wa Mkoa amewashukuru viongozi hao kwa kukutana nae na kuwaomba kuisaidia Serikali katika kukemea maovu mbalimbali katika jamii ikiwemo kukemea wananchi wanapochukua sheria mkononi kunapokuwa na jambo ambalo linaweza kutatuliwa kwa kufuata sheria na taratibu za nchi.  

“Ninawaomba katika mahubiri yenu kukemea vitendo viovu katika jamii ikiwa ni pamoja na mauaji ya mara kwa mara yasiyo na sababu za msingi ambayo yapo katika jamii na kupunguza ukatili kwa kupigana kwa kutumia silaha katika migogoro ya kifamilia na kijamii” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amewaomba viongozi wa dini kukemea na kuliweka katika maombi suala la ulawiti na ubakaji wa watoto wadogo mashuleni na katika jamii na kukemea migogoro ya ardhi inayosababishwa na ongezeko la idadi ya watu, mifugo na shughuli za kibinadamu katika ardhi iliyopo.

Aidha, Mhe. Mtambi amewataka viongozi hao kukemea kilimo cha madawa ya kulevya aina ya bangi na mirungi kinachofanywa na baadhi ya wananchi katika Mkoa wa Mara kwani madhara yake katika jamii ni makubwa sana.  

Mhe. Mtambi amesema kuanzia sasa, Kamati hiyo itakuwa na kikao na Mkuu wa Mkoa kila mwezi kujadili masuala mbalimbali na itaanzisha maombi ya pamoja ya kuliombea Taifa, viongozi na Mkoa wa Mara na wananchi wake.

Kwa upande wake, Katibu wa Kamati ya Amani na Maridhiano Mkoa wa Mara Shehe Juma Masiloli akisoma taarifa ya kamati hiyo amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Mara kwa kuaminiwa na kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Shehe Masiloli pia alitumia fursa hiyo kuwasilisha maombi ya Kamati hiyo ya kupatiwa shilingi 1,000,000 kwa ajili ya pango la ofisi na mafuta lita 140 kwa ajili ya ziara watakayoifanya katika Wilaya tatu za Mkoa wa Mara.

Aidha, Shehe Masiloli pia ameeleza kuwa baadhi ya viongozi wa taasisi za Serikali hawatoi ushirikiano kwa Kamati ya Amani na Maridhiano jambo ambalo linawawia vigumu kutekeleza majukumu yao na kuomba Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kuwawezesha wanapohudhuria vikao vya kamati hiyo kitaifa.

Kikao hicho pia kilihudhuriwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Askofu Jacob Lutubija na wajumbe wengine wa Kamati hiyo pamoja na baadhi ya maofisa wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa