• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

RAS aongoza makabidhiano ya magari yaliyotolewa na Amref

Posted on: March 5th, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara leo tarehe 05 Machi, 2025 ameongoza hafla ya kukabidhi magari matatu yaliyotolewa na Shirika llisilo la kiserikali la Amref kwa ajili ya kusaidia shughuli za usimamizi wa sekta ya afya katika Mkoa wa Mara.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi magari hayo, Bwana kusaya amewataka maafisa wanaokabidhiwa magari hayo kuyatumia vizuri kwenye shughuli za usimamizi wa sekta ya afya zilizokusudiwa na Shirika la Amref.

“Mimi nitafuatilia kwa karibu matumizi ya magari haya ili yatumike kwa makusudio yaliyopangwa ikiwa ni pamoja na kufuatilia muda wa matengenezo” amesema Bwana Kusaya.

Bwana Kusaya amelishukuru Shirika la Amref kwa kutoa msaada wa magari hayo na ni nyenzo muhimu katika utoaji wa huduma bora za afya kwa wananchi wa Mkoa wa Mara na kuahidi kuwa magari haya tutayatunza ili yaendelee kutoa huduma.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Afya Dkt. Zabroni Masatu amesema kuwa magari yaliyopokelewa ni Nissan Patrol moja kwa ajili ya matumizi ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara na magari mawili Toyota hardtop ambayo yamekabidhiwa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma na Halmashauri ya Mji wa Bunda.

Dkt. Masatu amelishukuru Shirika la Amref kwa msaada huo na kusema kuwa mahitaji ya magari ya usimamizi wa shughuli mbalimbali ya sekta za afya ikiwa ni pamoja na ukaguzi wa miradi ya sekta hiyo na vituo vya kutolea huduma za afya.

Kwa upande wake, Meneja wa Mradi wa Mkoa wa Mara Dkt. Revocatus Masanja amesema Amref imetoa magari matatu yaliyokuwa yanatumika kwa ajili ya usimamizi wa mradi wa ukimwi katika Mkoa wa Mara kwa ajili ya Halmashauri na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara kutokana na shirika hilo kuona mahitaji.

“Magari haya bado ni mazima yakitumika vizuri yatasaidia kutatua uhaba wa changamoto za magari kwa ajili ya usimamizi wa vituo vya kutolea huduma za afya na miradi ya sekta ya afya” amesema Dkt. Masanja.

Dkt. Masanja ameishukuru Serikali ya Mkoa wa Mara kwa ushirikiano mkubwa ambao umekuwa ukitoa kwa wadau mbalimbali ikiwemo Shirika la Amref na kuupongeza Mkoa kwa kujali afya za wananchi wake.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma Bwana Msongera Palera amelishukuru Shirika la Amref kwa kutoa msaada huo ambao utatatua upunguvu mkubwa wa magari katika Halmashauri hiyo.

“Awali tulikuwa tunaazima magari Amref mara kwa mara na sasa wameona watupatie gari moja iwe ya kwetu ili tuweze kuwahudumia wananchi vizuri zaidi” amesema Bwana Palera.

Bwana Palera amesema Halmashauri yao ina eneo kubwa sana na inavituo vingi vya kutolea huduma za afya kwenye vimesambaa maeneo mbalimbali ya Halmashauri hiyo na inakuwa vigumu kwa wasimamizi wa sekta ya afya kama hawana usafiri wa uhakika.

Hafla ya mapokezi ya magari hayo imehudhuriwa na baadhi ya watumishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, wenyeviti wa Halmashauri, Wakurugenzi wa Halmashauri, Wakuu wa Divisheni za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe wa Halmashauri hizo.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Rorya wahimizwa kutumia nishati safi ya kupikia

    August 19, 2025
  • Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa awasha Mwenge wa Mwitongo kwa mara ya 61

    August 18, 2025
  • Mwenge wakagua miradi ya bilioni 6 Musoma

    August 18, 2025
  • Maambukizi ya UKIMWI katika Wilaya ya Bunda yamepungua

    August 16, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa