• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Rais Samia aridhishwa na mapokezi Mara

Posted on: February 4th, 2022

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan leo ameingia Mkoani Mara na kuelezea kuridhishwa kwake na mapokezi makubwa aliyoyapata ambapo kimkoa amepokelewa katika Mji wa Bunda.

“Ingekuwa hamkuja kwa wingi hivi, ningesema sijakaribishwa Mkoa wa Mara, lakini kwa kuja kwenu kwa wingi hivi mmenikaribisha katika Mkoa wa Mara, Asanteni sana” alisema Mheshimiwa Rais.  

Mara baada ya kupokelewa katika Mji wa Bunda, Mheshimiwa Rais amesalimiana na wananchi wa Mji wa Bunda na baadaye kusalimiana na wananchi wa eneo la Kiabakari katika Wilaya ya Butiama.

Akizungumza mara baada ya kupokelewa katika Mji wa Bunda, Mheshimiwa Rais ameshukuru kwa mapokezi makubwa aliyoyapata katika Mkoa wa Mara.

“Kwa umati huu wa watu nimefurahi tumepokelewa vizuri katika Mkoa wa Mara.

Akizungumza wakati wa mapokezi ya Mhehsimiwa Rais, Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi amemkaribisha Rais katika Mkoa wa Mara.

“Wananchi wa Mkoa wa Mara wanakupenda sana na wanaridhika na kazi kubwa inayofanywa na serikali yako ya awamu ya sita” ameeleza Mheshimiwa Hapi.

“Kwa niaba ya viongozi wenzangu ndani ya Mkoa, sisi tunakupenda, tunakuamini, tunakuombea na tutakusaidia kutimiza maono yako kwa wananchi wa Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa wananchi wa Mkoa wa Mara wanafahamu kazi kubwa anayoifanya katika Mkoa wa Mara na umati wa wananchi uliojitokeza unadhihirisha mapenzi makubwa walionayo wananchi kwa Mheshimiwa Rais na serikali yake.

Kesho tarehe 5 Februari, 2022, Mheshimiwa Rais anatarajiwa kushiriki katika Matembezi ya Mshikamano ambayo yataanzia Ikulu Ndogo ya Mkoa wa Mara hadi katika Ofisi za CCM Mkoa wa Mara na baadaye Mheshimiwa Rais atakuwa Mgeni Rasmi katika kilele cha maadhimisho ya miaka 45 ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ambayo kitaifa yatafanyika katika Uwanja wa Karume, Manispaa ya Musoma.  

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, tarehe 6 Februari, 2022 Mheshimiwa Rais anataweka jiwe la msingi katika Mradi wa Maji wa Mgango- Kiabakari pamoja na kuwasalimia wananchi wa eneo la Mgango lililopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma.

Aidha siku hiyo Mheshimiwa Rais anatarajiwa kuweka jiwe la msingi katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (Kwangwa) iliyopo katika Manispaa ya Musoma na kuzungumza na wananchi wa eneo la Kwangwa.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa tarehe 7 Februari, 2022 Mheshimiwa Rais anatarajiwa kutembelea nyumbani kwa Baba wa Taifa katika eneo la Mwitongo, Wilayani Butiama na baadaye kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa ujenzi wa chujio la maji, katika Mradi wa Maji wa Bunda, liliopo katika eneo la Nyabehu, Wilaya ya Bunda.

Imeeleza pia kuwa Mheshimiwa Rais atahitimisha ziara yake kwa kuzungumza na wananchi wa Mji wa Bunda katika mkutano wa hadhara utakaofanyika katika viwanja vya sabasaba.  

Aidha Mheshimiwa Hapi amewaalika Watanzania wote kujitokeza kwa wingi katika Maadhimisho ya Miaka 45 ya CCM ambapo Mkoa wa Mara umepewa heshima wa kuwa mwenyeji wa tukio hilo la kihistoria kwa Chama cha Mapinduzi. 

Hii ni ziara ya kwanza ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan tangu alivyoapishwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 19 Machi 2020.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Rorya wahimizwa kutumia nishati safi ya kupikia

    August 19, 2025
  • Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa awasha Mwenge wa Mwitongo kwa mara ya 61

    August 18, 2025
  • Mwenge wakagua miradi ya bilioni 6 Musoma

    August 18, 2025
  • Maambukizi ya UKIMWI katika Wilaya ya Bunda yamepungua

    August 16, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa