• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Pongezi kwa Sekta ya Afya

Posted on: July 27th, 2020

Katibu Tawala Mkoa wa Mara Bibi Karolina Mthapula amewapongeza watumishi wote wa sekta ya Afya wa Mkoa wa Mara kwa kazi nzuri wanayoifanya hususan katika udhibiti wa janga la Corona.

Bibi Mthapula ameeleza hayo leo tarehe 25 Julai 2020 katika mji wa Tarime wakati akifunga mafunzo ya timu ya usimamizi wa huduma za afya katika Mkoa wa Mara yaliyotolewa kwa ushirikiano na Shirika la Misaada ya Maendeleo la Marekani (USAID) Boresha Afya.

“Pamoja na Mkoa wetu kuwa mpakani lakini kutokana na kazi kubwa mliyoifanya, Mkoa wa Mara hatukupata kabisa wagonjwa kutokea nchi jirani ambazo nyingi zimeathirika zaidi.

Hata hivyo amewataka wataalamu wa afya kuendelea kuhamasisha kuhusiana na tahadhari za kujikinga na Corona kwani watu wameanza kuacha kuchukua tahadhari.

Aidha amewapongeza wataalamu wa afya kwa usimamizi wa ujenzi wa hospitali na vituo vya afya katika Mkoa wa Mara ambavyo vimejengwa katika Mkoa wa Mara katika kipindi hiki cha awamu ya tano.

“Ninawaomba wale ambao wanavituo au hospitali ambazo hazijaanza kutoa huduma waanze mapema iwezekanavyo ili wananchi waweze kupata huduma zilizokusudiwa” alisema Bibi Mthapula.

Aidha amewataka wataalamu hao kujiandaa na kuziba pengo litakalobakia baada ya mradi huo Boresha Afya kukamilisha shughuli zake mwaka 2021.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt. Florian Tinuga amemshukuru Katibu Tawala kwa kuweza kuhudhuria sehemu ya mafunzo hayo pamoja na kuyafunga rasmi.

Aidha amewataka Waganga wa Halmashauri kukamilisha miradi mbalimbali ya ujenzi wa vituo vya afya na hospitali kama walivyoahidi ili kuweza kuanza kutoa huduma kwa wananchi.

“Hamna maana kwa serikali kutoa fedha kujenga vituo hivi kama wananchi hawapati huduma za afya kama ilivyokusudiwa” alisema Dkt. Tinuga.

 

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Tumieni magari haya kutatua kero za wananchi- Mtambi

    May 22, 2025
  • CCM yapongeza utekelezaji wa ilani ya uchaguzi Mara

    May 20, 2025
  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa