• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mwenge wa Uhuru wakamilisha Mbio zake Mara

Posted on: June 27th, 2021

Mwenge wa Uhuru leo tarehe 27 Juni 2021 umekamilisha mbio zake katika Mkoa wa Mara kwa kuhitimisha mbio zake katika Wilaya ya Bunda.

Kwa sasa Mwenge wa Uhuru leo ikiwa ni siku ya mwisho kuwa Mkoani Mara unaendelea na mkesha unaofanyika katika Chuo cha Ualimu Bunda.

Akizungumza baada ya chakula cha jioni Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Maalum mwaka 2021 Lt. Josephine Paul Mwambashi ameshukuru kwa mapokezi na ushirikiano walioupata wakiwa katika Mkoa wa Mara.

“Tumepata ushirikiano kutoka kwa viongozi na wananchi ambao umerahisisha ukaguzi wa miradi na mbio za mwenge kwenda vizuri bila tatizo lolote” alisema Mwambashi.

Mwenge wa Uhuru ukiwa katika Wilaya ya Bunda, umepokelewa katika stendi ya mabasi ya Nyamswa na baada ya hapo ukatembelea mradi wa ukusanyaji wa mapato katika vituo vya kutolea huduma za afya (GOTHOMIS) katika Kituo cha Afya Ikizu na kuweka jiwe la msingi katika mradi wa madarasa mawili katika Shule ya Sekondari ya Hunyari.

Aidha Mwenge wa Uhuru umetembelea mradi wa maji wa Kihumbu na umetembelea na kukagua Jukwaa la kielektroniki wa utoaji wa huduma za ugani na masoko kwa wakulima (M-Kilimo) na mfumo wa malipo ya mauzo ya pamba kwa njia ya kielektroniki.

Mwenge wa uhuru pia umeweka jiwe la msingi katika mradi wa Zahanati ya Mary Imaculate uliopo katika eneo la Bunda Stoo, umetembelea mradi wa ujasiliamali wa vijana wa utengenezaji mapambo na mikoba, umezindua mradi wa kiwanda cha tofali cha Halmashauri ya Mji wa Bunda na kutembelea mradi wa ukarabati wa Chuo cha Ualimu Bunda.

Kesho tarehe 28 Juni 2021 asubuhi Mwenge wa  Uhuru unatarajiwa kukabidhiwa katika Mkoa wa Simiyu tayari kwa kuendelea na mbio zake mkoani humo.

Mwenge wa Uhuru uliwashwa tarehe 17 Mei 2021 katika Mkoa wa Kusini Unguja na unatarajiwa kukamilisha mbio zake katika Wilaya ya Chato Mkoani Geita tarehe 14 Oktoba 2021.   

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa