• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

MTHAPULA: Wanawake changamkieni mikopo ya halmashauri

Posted on: March 8th, 2021

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bibi Karolina Mthapula amewataka wanawake wa Manispaa ya Musoma kuchangamkia mikopo ya wanawake inayotolewa na halmashauri yenye lengo la kuwakomboa kiuchumi.

Mama Mthapula ametoa kauli hiyo leo tarehe 8 Machi 2021 alipokuwa Mgeni Rasmi katika kongamano la Siku ya Wanawake Duniani katika Manispaa ya Musoma lililofanyika katika Ukumbi wa MCC uliopo ndani ya eneo la Chuo Kikuu Huria, katika mji wa Musoma.

“Tunaishukuru sana serikali kwa kutenga asilimia nne ya mapato ya ndani kutolewa kama mikopo isiyokuwa na riba kwa wanawake waliojiunga katika vikundi vya uzalishajimali na ujasiriamali” alisema Bibi Mthapula.

Mheshimiwa Mthapula ameeleza kuwa mikopo hiyo ambayo inatolewa kama sehemu ya mapato ya ndani ya halmashauri kwa mujibu wa sheria haina riba yoyote, wanawake wanatakiwa kuichukua na kurejesha mapema ili wenzao pia waje wakope.

Aidha ametoa wito kwa wanawake kushiriki katika malezi bora ya watoto katika ngazi ya familia na jamii kwa ujumla ili kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

Amempongeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Musoma kwa maandalizi mazuri ya kongamano hilo na kushirikisha wanawake wa aina tofauti tofauti katika kongamano hilo.  

Kwa Upande wake Meya wa Manispaa ya Musoma Mheshimiwa Patrick William Gumbo amewataka wanawake kupendana na kusaidiana katika kufikia malengo yao.

“Ninaomba kuwasihi wanawake msaidiane na mwanamke mmoja akipanda awe daraja la kuwavusha wananwake wengine waweze kupanda pia” alisema Mheshimiwa Gumbo.

Ameeleza kuwa haki ya wananwake ipo lakini wanahitaji kuitafuta hawataipata bila mapambano na katika mapambano hayo ushirikiano wa wao kwa wao ni muhimu sana.

Ameeleza kuwa katika Mkoa wa Mara kuna Katibu Tawala mwanamke, wakuu wa wilaya wawili wananwake na wakurugenzi wa halmashauri watatu ni wananwake, wakitumika vizuri wanaweza kuwavusha wanawake wengi zaidi kupata nafasi za uongozi.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Msoma Bibi Fidelica Myovella ameeleza amewahimiza wanawake kuchangamkia mikopo isiyo na riba inayotolewa na halmashauri ili kuinua hali yao ya kiuchumi.

Bibi Myovella ameeleza kuwa katika Manispaa ya Musoma kuanzia mwaka 2018/2019 hadi Desemba 2020 vikundi vya wanawake 150 na wanafuika 660 wamepata mkopo unaotolewa na Manispaa kwa ajili ya wananwake.

Aidha Bibi Myovella ameeleza kuwa maadhimisho ya siku ya wanawake Manispaa ya Musoma yalianza tarehe 7 Machi 2021 ambapo manispaa iliandaa bonanza la michezo kwa ajili ya waheshimiwa madiwani na washindi wa bonanza hilo walipata zawadi.

Kauli mbiu ya siku ya wananwake duniani mwaka huu ni Wanawake katika Uongozi, Chachu ya kufikia Dunia yenye Usawa.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa