• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi awataka wananchi kuchangamkia fursa ya Madaktari Bingwa

Posted on: November 11th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi leo amepokea awamu ya pili ya Madaktari Bingwa 63 wa Mama Samia na kuwataka wananchi wa Mkoa wa Mara kuchangamkia fursa za uwepo wa Madaktari Bingwa kupata huduma za kibingwa katika maeneo yao.

Akizungumza katika mapokezi hayo, Mhe. Mtambi amesema Serikali imewasaidia wananchi na badala ya wagonjwa kwenda kwenye hospitali za rufaa ambazo zipo mbali kupata huduma za kibingwa, wanapata huduma za kibingwa na kibobezi katika maeneo yao baada ya Serikali kufanya maboresho makubwa katika sekta ya afya.  

“Hii imewezekana kwa sababu Serikali imeboresha miundombinu na vifaa tiba na watumishi katika Hospitali za Halmashauri na vituo vya afya na kuwezesha madaktari bingwa kuweza kutoa huduma katika Hospitali hizo” amesema Mhe. Mtambi.

Mhe. Mtambi amesema madaktari hawa watatoa huduma katika Hospitali ya Manispaa ya Musoma, Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Tarime, Hospitali ya Nyamwaga, Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti na Hospitali ya Wilaya ya Rorya.

Aidha, madakatari hao watatoa pia huduma katika Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Butiama, Hospitali ya Manyamanyama (Bunda Mjini), Kituo cha Afya Ikizu na Kituo cha Afya Kasahunga vilivyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.

Kwa mujibu wa Mhe. Mtambi magonjwa yatakayotibiwa na madaktari hawa ni magonjwa ya wanawake na uzazi, watoto na watoto wachanga, magonjwa ya ndani kama vile kisukari, presha na kadhalika, upasuaji na matatizo ya mfumo wa mkojo na magonjwa ya kinywa na meno.

Mhe. Mtambi ametoa rai kwa wataalamu wa afya wa Mkoa wa Mara kusimamia na kuratibu vizuri zoezi hili ili wananchi wenye changamoto waweze kupata huduma stahiki na kwa wakati na kwa kuzingatia maelekezo na miongozo ya Serikali.  

Mhe. Mtambi amewakaribisha sana madaktari bingwa katika Mkoa wa Mara na kuwataka kabla ya kuondoka watembelea kaburi la Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na kula nyama choma na kichuri katika Mkoa wa Mara.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Wizara ya Afya Dkt. Joakim Masunga ameeleza kuwa Halmashauri zote zimepangiwa Madaktari Bingwa na Wauguzi Bingwa watakaosaidia kutoa huduma za kibingwa kwa wananchi kulingana na mahitaji.

Dkt. Masunga ameeleza kuwa madaktari hao wanatarajiwa kuanza kutoa huduma kuanzia leo hadi tarehe 16 Novemba, 2024 na wanategemewa kutumia muda wao kushughulikia matatizo mbalimbali ya wagonjwa.

Dkt. Masunga amesema madaktari hao bingwa wakiwa katika Hospitali hizo watawajengea uwezo watumishi wa sekta ya afya katika maeneo mbalimbali, watasaidia kupunguza rufaa za wagonjwa na kuongeza mapato ya hospitali hizo.

Dkt. Masunga ameeleza kuwa madaktari hao watatoa huduma katika vituo hivyo kuanzia tarehe 11 Novemba, 2024 hadi tarehe 16 Novemba, 2024 na watafanya kazi katika muda wa kawaida wa kazi wa hospitali za Halmashauri na vituo vya afya.

 Hafla mapokezi ya madaktari hayo imehudhuriwa pia na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Gerald Musabila Kusaya, Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Menejimenti ya Sektretarieti ya Mkoa wa Mara, Katibu Tawala wa Wilaya ya Musoma, Wakurugenzi wa Halmashauri, Timu ya Usimamizi wa Sekta ya Afya Mkoa wa Mara (RHMT) na Waganga Wakuu wa Halmashauri.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa