• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

Posted on: May 8th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Evans Alfred Mtambi leo amefungua kongamano la Jukwaa la Ushirika Mkoa wa Mara na kuwataka viongozi wa vyama vya ushirika kuongeza ubunifu katika kutumia fursa zilizopo ili kujenga uchumi wa wanaushirika.

Akizungumza katika hafla ya ufunguzi iliyofanyika katika ukumbi wa Mwembeni Complex, Manispaa ya Musoma Mhe. Mtambi amesema ushirika ukitumiwa vizuri unaweza kumaliza tatizo la upatikanaji wa mtaji wa biashara katika sekta mbalimbali.

“Kwa sasa Serikali ya Mkoa wa Mara inasimamia uendeshaji wa vyama vya ushirika kwa karibu sana na niwatahadharishe tu viongozi kutojihusisha na ubadhilifu wa mali za ushirika, huo utakuwa ni sawa na uhujumu uchumi, hatutakubali hilo litokee na likitokea hatua kali za kisheria zitachukuliwa”amesema Mhe. Mtambi.

Aidha, amewataka viongozi wa vyama vya ushirika kwa kushirikiana na wataalamu wa kilimo kuchukua hatua za kudhibiti utoroshaji wa mazao ya kimkakati ikiwa ni pamoja na kusimamia uuzaji wa mazao kupitia mfumo wa skatabadhi ghalani ili uweze kutumika katika ununuzi wa mazao mengi ya wananchi.

Mhe. Mtambi amesema suala la vyama kujiunga kwenye mfumo wa MUVU sio la hiari na kutoa hadi tarehe 30 Juni, 2025 vyama vyote vya ushirika Mkoa wa Mara viwe vimejiunga na mfumo wa MUVU na kuwataka Wakuu wa Wilaya kufuatilia utekelezaji wa suala hilo.

Aidha, ametumia fursa hiyo kuwahamasisha wanaushirika wa Mkoa wa Mara kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 ili kuwachagua viongozi watakaoliletea maendeleo Taifa la Tanzania.

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Jukwaa la Ushirika Mkoa wa Mara Bwana Samwel Gisiboye akisoma risala ya jukwaa hilo amesema Mkoa wa Mara una jumla ya wanachama 21,963 na wasio wanachama 11,665 wanaohudumiwa na vyama vya ushirika.

Bwana Gisiboye amesema Mkoa wa Mara una jumla ya vyama vya ushirika 308 lakini kati ya hivyo vyama vya ushirika 283 tu ndio vimesajiriwa katika mfumo wa MUVU na maafisa ushirika 11 huku kukiwa na upungufu wa maafisa ushirika 12 ii kuhudumia wanaushirika wa Mkoa wa Mara.

“Vyama vya akiba na Mikopo (SACCOS) katika Mkoa wa Mara vina mtaji wenye thamani ya shilingi 5, 280,008,536 na vimewezesha mikopo ya shilingi 6,395,015,531 kwa wananchama wake” amesema Bwana Gisiboye.

Bwana Gisiboye amesema vyama vya ushirika vimewekeza katika miradi mbalimbali yenye thamani ya shilingi 28,281,953,062.67 na kuwezesha utoaji wa ajira za 490 za kudumu na za muda na jumla ya shilingi 29,000,000 kimewekezwa katika Hisa za Benki ya Ushirika Tanzania (COOP Bank).

Bwana Gisiboye ameelezea manufaa waliyopata wakulima wa Choroko katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Halmashauri ya Mji wa Bunda na Halmashauri ya Wilaya ya Musoma ambao waliuza mazao yao kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani na bei ya zao hilo imeongezeka karibia mara mbili kwa kilo moja.  

Amesema dira ya Jukwaa la Ushirika katika Mkoa wa Mara ni kuwa na baraza huru, imara na endelevu la wanaushirika lenye taswira ya kuche hemusha maendeleo ya kiuchumi na kijamii.  

Ufunguzi wa kongamano hilo limehudhuriwa na Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Mrajisi Msaidizi wa Vyama vya Ushirika, wawakilishi kutoka Benki ya Ushirika Tanzania, wadau wa ushirika na viongozi wa vyama vya ushirika.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mtambi alitaka jukwaa la ushirika kuongeza ubunifu

    May 08, 2025
  • Jumuiya ya Waislamu Musoma yachangia madawati

    May 08, 2025
  • Kusaya apokea vifaa vya mapambano dhidi ya HIV/UKIMWI

    May 06, 2025
  • Mtambi ataka elimu zaidi kutunza Maeneo ya Urithi wa Dunia

    May 06, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa