• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Milioni 100 Kuboresha Barabara ya Hospitali ya Serengeti

Posted on: April 28th, 2020

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhandisi Joseph Nyamhanga ameahidi kutoa shilingi milioni 100 kujenga barabara kwa kiwango cha changarawe ya kuelekea katika Hospitali ya Wilaya ya Serengeti.

Akizungumza leo tarehe 21 Aprili 2020 baada ya kupokea taarifa na kukagua hospitali ya Wilaya ya Serengeti, Eng. Nyamhanga ameeleza kuwa kwa sasa ofisi yake itatoa fedha hizo ili kuwawezesha wagonjwa, watumishi na wananchi kupita sehemu nzuri wakati serikali inatafuta fedha za kujenga kwa kiwango cha lami.

“TAMISEMI itatoa milioni 100 ili kujenga barabara hii mapema iwezekanavyo ili kuifanya barabara hii ipitike kiurahisi” alisema Nyamhanga.  

Aidha Eng. Nyamhanga amepongeza ubunifu uliofanywa na Wilaya ya Serengeti wa kuweka wodi za muda katika jengo la wagonjwa wa nje. “Huu ni ubunifu mzuri sana kwani unahakikisha wananchi wanapata huduma wakati hospitali ikiendelea kukamilishwa”.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Dkt. Emiliana Donald ameeleza kuwa awamu ya kwanza ya ujenzi wa hospitali hiyo umekamilika na kwa sasa hospitali imeanza kutumika kutoa huduma za afya kwa wananchi.

“Majengo ya awamu ya kwanza yaliyokamilika na yanayotoa huduma ni pamoja na majengo ya mama na mtoto,  utawala, kusubiria wagonjwa, lango la kuingilia hospitali, jengo la wagonjwa wa nje pamoja na barabara ya kuunganisha majengo ya hospitali” alisema Dkt. Donald.

Aidha kwa sasa hospitali hiyo inajumla ya watumishi 56 tu ambao ni nusu ya watumishi wanaohitajika kukidhi mahitaji ya Hospitali za Wilaya.

Aidha alizitaja changamoto zinazoikabili hospitali hiyo kwa sasa ni pamoja na maji, ukosefu wa wodi za kulaza wagonjwa, nyumba za watumishi, jengo la mionzi, mochwari na kichomea taka.  

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Mheshimiwa Nurdin Babu ameeleza kuwa hospitali hiyo kwa sasa inakabiliwa na changamoto kubwa ya uchakavu wa barabara ya kuingia hospitali hiyo yenye urefu wa zaidi ya kilomita 3.

“Kwa sasa ili kuja kwenye hospitali hii, baada ya kumaliza lami tunalazimika kupita kwenye mashamba ya wananchi ili kukwepa madimbwi yaliyopo kwenye barabara hii” alisema Mheshimiwa Babu.

Mheshimiwa Babu alisema changamoto nyingine za hospitali hiyo ni pamojana gari ya kubebea wagonjwa, uzio wa kuzunguka hospitali hiyo na upungufu wa miundombinu  hususan wodi za wagonjwa.

Mheshimiwa Babu alisema awamu ya kwanza ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Serengeti ulianza mwaka 1974 kwa michango ya wananchi na wadau mbalimbali, lakini ujenzi huo ulimaliziwa na fedha za serikali ya Awamu ya Tano na hivi sasa umekamilika na wameanza kutoa huduma.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • Waongozeni wanafunzi kufikia ndoto zao- Kusaya

    May 29, 2025
  • Kamati za Maafa Mkoa wa Mara zajengewa Uwezo

    May 26, 2025
  • Kikwete achangisha milioni 200 za ujenzi wa kanisa Mara

    May 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa