• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Sehemu ya Mipango na Uratibu
      • Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
      • Sehemu ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Sehemu ya Uratibu wa Sekta ya Uchumi na Uzalishaji
      • Sehemu ya Utawala na usimamizi wa rasilimali watu
      • Sehemu ya Huduma za Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
      • Sehemu ya usimamizi, ufuatiliaji na ukaguzi
      • Sehemu ya Miundombinu
    • Vitengo
      • Kitengo cha Huduma za Kisheria
      • Kitengo cha Uhasibu na Fedha
      • Kitengo cha Ukaguzi wa ndani
      • Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
      • Kitengo cha Maendeleo ya Jamii
      • Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara Yazindua unyunyuziaji magari dawa

Posted on: April 17th, 2020

16 Aprili 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima leo amezindua zoezi la kunyunyuzia dawa ya kudhibiti Corona kwenye magari ya abiria katika setendi kuu ya mabasi ya Bweri iliyopo Musoma Mjini.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa zoezi hilo Mheshimiwa Malima amewataka wamiliki wote wa magari ya abiria kuhakikisha kuwa magari yote yananyunyuziwa dawa kabla ya kuondoka stendi ili kuhakikisha usalama wa watumiaji wa magari hayo.

“Sisi kama serikali tuhakahikisha kila mmiliki na dereva wa magari anafuata utaratibu tuliojiwekea katika Mkoa wa Mara ili kuendelea kuwakinga watu wanaotumia magari haya” alisema Malima.

Aidha aliwahimiza wananchi wote kufuatilia maelekezo yote ya wataalamu wa afya ikiwa ni pamoja na kunawa mikono, kuchukua tahadhari mbalimbali za kujikinga.

“Suala la kunawa mikono kwa sabuni na maji tiririka ni muhimu sana wakati huu na japokuwa linaonekana ni jambo rahisi likifanyiwa mzaha litawaathiri watu wengi zaidi.”

Wakati huo huo, Mkuu wa Mkoa akiwa stendi ya Bweri alipokea malalamiko kutoka kwa wananchi kuhusu shida ya upatikanaji wa maji katika eneo hilo.

Akijibu malalamiko hayo, Mheshimiwa Malima amewataka Mamlaka ya Maji Musoma (MUWASA) kuhakikisha maji yanapatikana kwa urahisi katika stendi hiyo ili kuwanusuru wananchi na wasafiri wanaotumia stendi hiyo kujikinga na corona na magonjwa mengine ya mlipuko.

Mkuu wa Mkoa katika uzinduzi huo aliambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, viongozi wa wilaya ya Musoma Mjini na Halmashauri ya Manispaa ya Musoma.  

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mara Dkt. Florian Tinuga alisema zoezi hilo litafanywa katika stendi zote za Mkoa wa Mara kuanzia tarehe 16 Aprili 2020.

Aidha ameeleza kuwa utaratibu unataka magari kunyunyuziwa dawa nusu saa kabla ya kuanza kupakia abiria katika magari hayo.

“Hatua hii ni muhimu kwa ajili ya kuwalinda abiria na wafanyakazi wa magari haya ambao wanakutana na watu wengi waliotoka sehemu mbalimbali ili waweze kujilinda na corona” alisema Dkt. Tinuga

 Katika utaratibu huu wa kupuliza magari dawa, wamiliki wa magari watatozwa shilingi 5000 kwa mabasi makubwa, 3000 kwa basi ndogo (coaster) na shilingi 2000 kwa mabasi madogo madogo.

Matangazo ya Kawaida

  • MBIO ZA MWENGE WA UHURU, 2025 August 11, 2025
  • HAFLA YA UTIAJI SAINI MKATABA YA TACTICS August 11, 2025
  • KONGAMANO LA VIJANA August 11, 2025
  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE 2017 January 31, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Rorya wahimizwa kutumia nishati safi ya kupikia

    August 19, 2025
  • Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa awasha Mwenge wa Mwitongo kwa mara ya 61

    August 18, 2025
  • Mwenge wakagua miradi ya bilioni 6 Musoma

    August 18, 2025
  • Maambukizi ya UKIMWI katika Wilaya ya Bunda yamepungua

    August 16, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa