• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yapokea vifaa vya kusafisha figo

Posted on: July 28th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Adam Kighoma Ali Malima amepokea vifaa vya tiba ya figo vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 300 kwa ajili ya kitengo cha Figo cha Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara.

Akizungumza katika hafla ya kupokea vifaa hivyo, Mheshimiwa Malima ameishukuru sana serikali kwa kuleta vitaa hivyo katika Mkoa wa Mara ambavyo vitaenda sambamba na uzinduzi wa Hospitali ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere ambayo inatarajia kuzinduliwa rasmi mwezi Agosti, 2020.

“Kwa niaba ya wananchi wa Mkoa wa Mara ninaishukuru sana serikali kwa kutupatia mashine hizi ambazo zimekuja kuimarisha Kitengo cha Figo katika hospitali hii ya Rufaa ya Mkoa wa Mara” ameeleza Mheshimiwa Malima.

Mheshimiwa Malima amemuagiza mhandisi mkazi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kuhakikisha anakamilisha sehemu zitakazofungwa mashine hizo kabla ya tarehe 30 Julai 2020 na kupunguza vizingizio katika utekelezaji wa mradi huo.

“Serikali imeleta pesa shilingi bilioni 4.1 za kukamilisha mradi huu, sasa fanyeni kazi usiku na mchana kukamilisha ili wananchi waanze kupatiwa huduma haraka iwezekanavyo” alisema Mheshimiwa Malima.

Aidha amemuagiza Katibu Tawala Msaidizi, Miundombinu Mhandisi Faustine Tarai kuhakikisha huduma za umeme, maji na barabara zinafika katika hospitali hiyo kabla ya tarehe 30 Julai 2020.

Kwa mujibu wa Mheshimiwa Malima kitengo cha Figo na sehemu ya Mama na Mtoto zinatarajiwa kuanza kutoa huduma ifikapo tarehe 15 Agosti, 2020 hivyo huduma hizo ni muhimu kuimarishwa mapema.

Kwa upande wake Mratibu wa Magonjwa yasiyoambukiza Dkt. Frederick Buswelo wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee ambaye alikabidhi vifaa hivyo kwa niaba ya serikali ameeleza kuwa vifaa vilivyoletwa ni Mashine tisa za kusafisha figo, vitanda tisa pamoja na vifaa vya kufundia mashine hizi.

Dkt. Biswalo ameeleza kuwa vifaa hivi ni sehemu ya mashine 62 zilizotolewa na Serikali ya Falme za Kiarabu aidha shirika moja la Ujerumani liliongeza nyingine ambazo zimegawiwa katika hospitali za rufaa mbalimbali Tanzania bara pamoja na Zanzibar.

Ameitaja baadhi ya hospitali za rufaa zilizopata mashine hizi ni pamoja na  Mara, Tanga, Mwanza, Kigoma, Mtwara na kadhalika na kuwa mpango wa serikali kupeleka mashine hizi katika hospitali za rufaa 20 ifikapo Novemba 2020.

“Upatikanaji wa vifaa hivi katika hospitali zetu za rufaa itapunguza sana gharama za kusafirisha wagonjwa kwenda nje ya nchi kupata huduma hizo na itaokoa vifo vingi sana hususan kwa wanawake wajawazito.

Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa Mkoa wa Mara Dkt. Joakim Enyembe ameeleza kuwa maandalizi ya kupokea vifaa hivi ikiwa ni pamoja na kuwaandaa watumishi watakaosimamia yamefanyika.

“Tayari hospitali imetoa wafanyakazi saba ambao wameshapatiwa mafunzo ya kuvtumia na baada ya kufungwa wataanza kuvitumia” alisema Dkt. Enyembe.

Ameeleza kuwa vifaa hivi vitaokoa maisha ya wananchi walio wengi katika Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Tumieni magari haya kutatua kero za wananchi- Mtambi

    May 22, 2025
  • CCM yapongeza utekelezaji wa ilani ya uchaguzi Mara

    May 20, 2025
  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa