• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mara yajipanga kuwa kinara wa elimu

Posted on: March 23rd, 2022

Mkoa wa Mara umeanza kuchukua hatua mbalimbali ili kuweza kufanya vizuri katika matokeo ya wanafunzi katika mitihani ya kitaifa ili kurejea katika nafasi yake ya zamani.

Hayo yameelezwa na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara, Bwana Benjamin Oganga, wakati akifungua mafunzo ya takwimu kwa walimu wa takwimu wa Shule za Msingi na Sekondari yanayofanyika katika Shule ya Sekondari ya Ufundi ya Musoma.

“Sio jadi yetu Mkoa wa Mara kufanya vibaya kwenye matokeo ya mitihani, mimi nimesoma Mkoa Mara elimu ya Msingi na Sekondari na Mkoa wa Mara wakati huo ulikuwa tunafanya vizuri sana, haiwezekani sasa tukawa tunafanya vibaya” alisema Oganga.  

Bwana Oganga ambaye pia ni Afisa Eimu wa Mkoa wa Mara ametumia nafasi hiyo kuwakumbusha walimu waliohudhuria mafunzo hayo kutimiza wajibu wao kwa kufundisha na kuwasimamia wanafunzi katika shule zao.

“Tumepewa dhamana kubwa sana, sisi ndio tunaotengeneza Tanzania, ukisikia viongozi ,  wakulima, wafanyabiashara, wafanyakazi wote wametengenezwa na walimu, tutimize wajibu wetu” alisema Bwana Oganga.  

Bwana Oganga ameeleza kuwa hakuna kazi isiyokuwa na changamoto, hivyo amewataka walimu kutimiza wajibu wao wakati serikali ikizifanyia kazi changamoto zilizopo katika sekta ya elimu ili kuboresha mazingira ya kufundisha na kujifunzia.  

Amewataka walimu kuongeza juhudi katika ufundishaji na ujifunzaji na Mkoa ukibaini kuwa Mwalimu hafundishi utachukua hatua kali ili iwe fundisho kwa walimu wengine.

Kuhusu mafunzo hayo, Bwana Oganga amewakumbusha walimu kuwa kazi ya takwimu wanayoifanya ni kazi ya kisheria na mafunzo hayo yanalengo la kuwajengea uwezo wa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.  

Bwana Oganga amewasistiza walimu hao kuhusu umakini katika ujazaji wa madodoso mbalimbali yanayoletwa na kuhakikisha usahihi wa takwimu hizo na kuyajaza madodoso na kuyarudisha kwa muda unaotakiwa.

“Tukisema madodoso haya yafike Halmashauri tarehe fulani, basi yajazwe kwa usahihi na yafike kwa tarehe hiyo au kabla ya tarehe husika” alisema Bwana Oganga.

Aidha Bwana Oganga amewataka Maafisa Elimu wa Halmashauri kuwaandikia barua rasmi za uteuzi kwa walimu wote walioshuriki katika mafunzo hayo kwa ajili ya kutekeleza majukumu hayo ikieleza majukumu yao kama walimu wa Takwimu katika shule zao.

Kwa upande wake, Afisa Elimu Taaluma wa Mkoa wa Mara Bwana Ayoub Mbilinyi, amemkaribisha Kaimu Katibu Tawala Mkoa kufungua mafunzo hayo.

Bwana Mbilinyi ameeleza kuwa mafunzo hayo ya siku moja yanawahusisha walimu wa Takwimu wa Shule za Msingi na Sekondari wa Halmashauri ya Wilaya ya Musoma na Manispaa ya Musoma  na kesho yataendelea katika halmashauri nyingine.  

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa