• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Makungu azindua Kituo cha Kuratibu M-MAMA Mara

Posted on: May 26th, 2023

Katibu Tawala Mkoa wa Mara Bwana Msalika Robert Makungu leo amezindua kituo cha kuratibu usafiri wa dharura kwa wajawazito, wazazi na watoto wachanga (M-MAMA) kwa Mkoa wa Mara katika Hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere iliyopo eneo la Kwangwa, Manispaa ya Musoma.

Akizungumza baada ya kuzindua kituo hicho, Bwana Msalika Makungu amewataka watumishi wa sekta ya afya watakaoratibu mfumo huo kuhakikisha wanatimiza wajibu wao kwa uadilifu ili kupunguza na hatimaye kutokomeza kabisa vifo vya Mama na Matoto vinavyotokana na kucheleweshwa kupata huduma za matibabu.

“Pamoja na uwekezaji mkubwa ambao serikali imefanya katika kujenga miundombinu, kununua dawa na vifaa tiba, kuajiri na kuwamotisha watumishi katika sekta ya afya, kama hatutafanya kazi kwa kuzingatia maadili, uadilifu na kuthamini uhai wa watu, vifo vitaendelea kuwepo” alisema Bwana Makungu.

Aidha, Bwana Msalika amezitaka Kamati za Usimamizi wa Afya  katika ngazi za Mkoa na Halmashauri kuhakikisha mfumo huo unasimamiwa vizuri na unaleta matokeo chanya katika maisha ya wananchi wa Mkoa wa Mara.

Bwana Makungu amewataka wananchi kuitumia namba 115 ya kuomba usafiri kwa kuzingatia madhumuni ya namba hiyo na hitaji la msingi la kuwasaidia wagonjwa wenye uhitaji wa dharura ili kuweza kuokoa maisha ya Mama na Mtoto.  

Akizungumza katika tukio hilo, Muuguzi Mkuu na Mratibu wa M-MAMA Mkoa wa Mara Bwana Stanley Kajuna ameeleza kuwa mpango wa M-Mama katika Mkoa wa Mara umezinduliwa rasmi tarehe 13 Februari, 2023 na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara Meja Jenerali Suleiman Mungiya Mzee.

Bwana Kajuna ameeleza kuwa baada ya uzinduzi shughuli mbalimbali zimefanyika kuruhusu maandalizi ya kuanza kutumika kwa mfumo huo ikiwa ni pamoja na kutambua magari na madereva wa jamii watakaotoa huduma, kuwafanyia mafunzo madereva na kuingia nao makubaliano rasmi.

Aidha, shughuli nyingine ilikuwa kuwatambua na kutoa mafunzo kwa wasimamizi wa mfumo, kuandaa chumba maalum kitakachotumika kuratibu usafiri wa dharura na kuweka nyenzo muhimu katika uratibu wa mfumo huo.

Uzinduzi huo umehudhuriwa na wawakilishi wa Vodacome Tanzania Foundation, Pathfinder International, Touch Foundation, wawakilishi wa Wizara ya Afya na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na baadhi ya wasimamizi wa mfumo huo kutoka Mkoa wa Mara.

M-MAMA ni mfumo wa Serikali ulioandaliwa kusaidia upatikanaji wa usafiri wa haraka wakati wa dharura wa kusafirisha wajawazito, wazazi na watoto wachanga wenye changamoto kutoka kituo kimoja kwenda kingine ili kupata matibabu zaidi ambayo hayawezi kupatikana katika kituo cha awali.

Mkoa wa Mara unakuwa Mkoa wa 17 kuanza kutumia mfumo huu tangu mfumo huu ulipozinduliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan tarehe 6 Aprili, 2023 Mkoani Dodoma na kuagiza mfumo huu kutumika nchi nzima.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wauguzi kuviishi viapo vyao

    May 30, 2025
  • Waongozeni wanafunzi kufikia ndoto zao- Kusaya

    May 29, 2025
  • Kamati za Maafa Mkoa wa Mara zajengewa Uwezo

    May 26, 2025
  • Kikwete achangisha milioni 200 za ujenzi wa kanisa Mara

    May 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa