• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Kusaya awataka Maafisa Elimu kusimamia utoaji wa chakula shuleni

Posted on: December 18th, 2024

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Gerald Musabila Kusaya leo ameongoza kikao cha Maafisa Elimu wa Halmashauri za Mkoa wa Mara na kuwataka Maafisa Elimu wa Halmashauri kusimamia kikamilifu suala la utoaji wa chakula shuleni kwa wanafunzi wa shule zote za kutwa.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao hicho, Bwana Kusaya amesema kwa sasa takwimu za kitaifa zinaonyesha kuwa asilimia 54.1 ya wanafunzi wote wa Mkoa wa Mara ndio wanapata chakula wakiwa shuleni jambo ambalo amesema halikubaliki.

“Fuatilieni michango ya wazazi na kama hawatoi kwa hiari zishaurini Halmashauri kutunga sheria ndogo ndogo ili kuwawezesha wazazi wa wanafunzi kuchangia kwa lazima na kuwawezesha wanafunzi wote wa kutwa kupata angalau mlo mmoja wakiwa shuleni” amesema Bwana Kusaya.  

Bwana Kusaya amezipongeza Halmashauri ambazo angalau zimejitahidi na kuzitaka Halmashauri zote kutoa chakula kwa wanafunzi wote bila kufanya ubaguzi kwa wanafunzi kutokana na wazazi wao kutokuchangia chakula.

Bwana Kusaya amesema utoaji wa chakula shuleni ni maagizo ya Serikali na kama Mkoa hautasita kuwachukulia hatua maafisa watakaozembea au kukwamisha utekelezaji wa maagizo haya yanayolenga kuboresha ufundishaji na ujifunzaji shuleni.

“Msitaka tuanze kufuatiliana kwenye utekelezaji wa jambo muhimu kama la utoaji wa chakula shuleni, timizeni wajibu wenu na mhakikishe watoto wote wanakula wawapo shuleni” amesema Bwana Kusaya.

Bwana Kusaya amesema utoaji wa chakula ni suala muhimu sana katika maendeleo ya elimu ya Tanzania na nchi isipokuwa na wananchi walioelimika inakuwa vigumu kwa nchi hiyo kupata maendeleo endelevu.  

Aidha, amewataka Maafisa Elimu kuwashirikisha viongozi wa Halmashauri zao na ofisi za Wakuu wa Wilaya katika uhamasishaji wa wazazi na walezi kuchangia chakula shuleni na kama kuna changamoto Mkoa pia utaarifiwe kuhusiana na changamoto za utekelezaji wa maagizo hayo ili uweze kuchukua hatua stahiki mapema.

Akizungumza katika kikao hicho, Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Bwana Makwasa Bulenga amesema kikao hicho cha Maafisa Elimu wa Halmashauri kinafanyika kila baada ya miezi miwili kikiwa na lengo la kufanya tathmini ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali.

Bwana Bulenga amesema katika kikao hicho kwa kuwa ni mwisho wa mwaka watafanya tathmini ya mambo yaliyofanyika katika kipindi cha mwaka mzima na kuweka mipango na mikakati ya utekelezaji wa shughuli kwa mwaka 2025.

Bwana Bulenga ametumia fursa hiyo kumuomba Katibu Tawala wa Mkoa kuangalia upya maombi ya uhamisho wa walimu kwa kuwa walimu wengi wanaomba kuhama kuliko wanaokuja katika Mkoa wa Mara.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Maafisa Elimu wote wa Halmashauri, Wadhibiti Ubora na baadhi ya Maafisa kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Mara na kimefanyika katika Ukumbi wa Uwekezaji uliopo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa