• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

hapi aongoza kikao cha maandalizi ya Mara Day 2021

Posted on: August 6th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi leo tarehe 5 Agosti 2021 ameongoza kikao cha maandalizi ya Siku ya Mara inayotarajia kufanyika tarehe 15 Septemba 2021 katika Wilaya ya Tarime.

Akizungumza katika kikao hicho Mheshimiwa Hapi amewataka wadau wa utalii na mazingira kuchangia maandalizi ya siku hiyo ili iweze kufana na kuwahamasisha wadau waweze kushiriki.

“Niwaombe wadau wote waweze kushiriki katika kuchangia maandalizi ya Siku ya Mara sio tu kwa fedha lakini hata kwa mawazo ili maadhimisho haya yaweze kuboreshwa na kuwa mazuri zaidi” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ameiagiza kamati ya maandalizi ya Siku ya Mara kuitangaza siku hiyo kitaifa na kimataifa ili kuimarisha jina la Mkoa wa Mara kwa wadau wake wa ndani na nje ya nchi.

Mheshimiwa Hapi amewataka Wakuu wa Wilaya kufufua siku za usafi na vikundi vya kufanya mazoezi katika wilaya zao ili kuimarisha afya za wananchi wa Mkoa wa Mara.

Aidha katika kutengeneza jina la Mkoa wa Mara, Mheshimiwa Hapi amesimamisha mashindano yote ya mbio yanayoitwa Serengeti katika Mkoa wa Mara hadi hapo Mkoa utakapopata mbio ambazo zitakazoutambulisha mkoa kitaifa na kimataifa.

Maadhimisho ya Siku ya Mara ni ya kimataifa yenye lengo la kuhamasisha utunzaji wa mazingira yanayouzunguka Mto Mara ambao unaanzia katika milima ya Mai nchini Kenya na kumwaga maji yake katika Ziwa Victoria katika Mkoa wa Mara.

Maadhimisho ya Siku ya Mara yanafanyika kila mwaka katika nchi za Kenya na Tanzania yakihusisha wadau mbalimbali hususa wadau wa utalii, maji na mazingira.  

Wakati huo huo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Bwana Albert Gabriel Msovela ameeleza kuwa Mkoa wa Mara pia unaandaa Maonyesho ya Teknolojia ya Madini na Wajasiriamali yatakayofanyika Oktoba 2021 katika eneo la Bweri nyuma ya stendi kuu ya mabasi.

Bwana Msovela ameeleza kuwa maonyesho hayo yatahusisha wadau wa madini na ujasiriamali kutoka katika Mikoa yote ya Kanda ya Ziwa ambayo ni Mara, Simiyu, Mwanza, Shinyanga, Kagera na Geita.

“Mpaka sasa tumeshapata eneo la ekari 10.3 kwa ajili ya maonyesho hayo na lipo katika eneo la Bweri katika Manispaa ya Musoma” alisema Bwana Msovela.

Ameeleza kuwa awali kulikuwa na mpango wa kuandaa maonyesho ya madini na baadaye likaja wazo la kuunganisha na wajasiriamali wadogo ili kuyapa nguvu zaidi maonyesho hayo.

Kikao kingine cha maandalizi ya shughuli hizi kinategemewa kufanyika tena tarehe 17 Agosti, 2021 katika ukumbi wa Uwekezaji uliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Tatueni kero za Wananchi- RC Mtambi

    July 03, 2025
  • Mara kuwawezesha wanawake kiuchumi kupunguza ukatili

    June 30, 2025
  • Mtambi afungua kambi ya madaktari bingwa na bobezi 64 Mara

    June 23, 2025
  • Watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa wa Mara wapatiwa mafunzo

    June 20, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa