• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Hapi aishukuru Benki NMB kwa msaada

Posted on: July 16th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi ameipongeza Benki ya NMB kwa msaada mkubwa uliyoitoa katika sekta za elimu na afya katika Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Hapi ametoa pongezi hizo wakati wa hafla fupi ya kupokea msaada huo iliyofanyika katika Shule ya Msingi Buhare iliyopo katika Manispaa ya Musoma leo tarehe 16 Julai 2021.

“Nimetaarifiwa kuwa NMB wametoa msaada wa vitanda, madawati, mabati na vifaa vya hospitali wenye jumla ya shilingi 140,000 katika Mkoa wa Mara, asanteni sana” amesema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa msaada uliotolewa katika Mkoa wa Mara ni mabati 2,580, madawati 937, vitanda nane kwa ajili ya Hospitali ya Rufaa Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere ambavyo vimegawiwa katika wilaya zote za Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa msaada uliotolewa na Benki ya NMB katika hafla hiyo ni sehemu ya msaada kubwa ambao wameutoa katika wilaya mbalimbali za Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa msaada huu unaendana na malengo ya Mkoa wa Mara na Serikali ya Awamu ya Sita kwa ujumla ya kuboresha huduma za jamii kwa wananchi wa Tanzania na hususan sekta za afya na elimu.

Aidha ameiomba Benki ya NMB kuendelea kutoa misaada ya hali na mali pale inapohitajika ili kuinua maendeleo ya Mkoa wa Mara.

Kwa upande wake, Mkuu wa Fedha wa Benki ya NMB Bwana Baraka Wenslaus ameeleza kuwa msaada uliotolewa ni sehemu ya fedha zaidi ya shilingi bilioni 2 ambazo zimetengwa na benki hiyo kama asilimia moja ya faida yake ya mwaka jana kwa ajili ya kuirudisha kwenye jamii.

“Mwaka jana Benki ya NMB ilipata faida ya shilingi bilioni 205 ambazo kwa mujibu wa sera za benki hiyo asilimia moja hurudishwa kwa jamii katika maeneo ya elimu, afya na elimu ya fedha na ujasiriamali kwa watanzania” ameeleza Bwana Wenslaus.

Ameeleza kuwa kwa Mkoa wa Mara wanamatumaini msaada walioutoa utaleta mabadiliko chanya na kuimarisha huduma za jamii katika sekta ya elimu na afya.

Katika hafla hiyo ya kupokea msaada, Mkuu wa Mkoa aliambatana na Mkuu wa Wilaya ya Musoma Dkt. Alfany Haule, Afisa Elimu wa Mkoa wa Mara, Meya na Mkurugenzi wa Manispaa ya Musoma, Mkurugenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara, viongozi wa CCM, walimu na wanafunzi.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa