• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

50,564 kufanya upimaji wa Kidato cha Pili Mara

Posted on: October 28th, 2024

Jumla ya wanafunzi 50,564 wanatarajiwa kufanya upimaji wa kitaifa wa Kidato cha Pili katika Mkoa wa Mara unaoanza leo tarehe 28 Oktoba, 2024 hadi tarehe 07 Novemba, 2024 kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA).

Taarifa iliyotolewa na Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Bwana Makwasa Bulenga imeeleza kuwa kati ya wanafunzi hao, wavulana ni 25,457 na wasichana ni 25,107 ambao wamo kwenye mikondo 1,309 katika shule za Sekondari 280 zilizopo katika Mkoa wa Mara.

Bwana Bulenga ameeleza kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime ina shule 47 zenye watahiniwa 7,333, Halmashauri ya Wilaya ya Rorya ina shule 53 zenye watahiniwa 7,005, Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti ina shule 44 zenye watahiniwa 6,704 huku Halmashauri ya Wilaya ya Butiama ikiwa na shule 31 zenye watahiniwa 6,101.

Halmashauri ya Wilaya ya Bunda ina shule 22 na watahiniwa 5,647, Halmashauri ya Wilaya ya Musoma ina shule 25 na watahiniwa 5,057, Manispaa ya Musoma ina shule 27 zenye watahiniwa 5,035, Halmashauri ya Mji wa Bunda ina shule 21 na watahiniwa 4,395 wakati Halmashauri ya Mji wa Tarime ina shule 16 na watahiniwa 3,287.

Bwana Bulenga ameeleza kuwa maandalizi yote ya upimaji huo yamekamilika ikiwemo semina za wasimamizi wa upimaji na vifaa vya upimaji tayari vimeshasambazwa katika Halmashauri zote tisa za Mkoa wa Mara.

Upimaji wa Kidato cha Pili unasimamiwa na Kamati za Uendeshaji za Mikoa/Halmashauri ambazo zimepewa mamlaka na Sheria ya Baraza la Mitihani sura 107 ya mwaka 1973 na marekebisho yake ya mwaka 2019.

Sekretarieti ya Mkoa wa Mara inawatakia wanafunzi wote wa Kidato cha Pili kila la kheri katika upimaji wa Taifa wa Kidato cha Pili.

Matangazo ya Kawaida

  • Ziara ya Waziri Mkuu February 24, 2024
  • MIAKA 60 YA MWENGE WA MWITONGO July 31, 2024
  • RC AIPOKEA KAMATI YA MADINI YA BUNGE February 25, 2024
  • SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASSA February 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Kusaya awataka wahanga kutumia misaada kuboresha maisha

    May 19, 2025
  • BASATA yaijengea uwezo Mkoa wa Mara

    May 15, 2025
  • Mara kutumia fursa zilizopo kuboresha sanaa kwa vijana

    May 15, 2025
  • RC aipongeza Musoma ushindi wa ubora wa huduma za afya Kitaifa

    May 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: 13 Barabara ya Boma, P.o.Box 299 Musoma, 31101 Musoma, Mara

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa