• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
MARA REGION

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mara

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Seksheni
      • Mipango na Uratibu
      • Sekta ya Elimu
      • Huduma ya Maji
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Serikali za Mitaa
      • Miundombinu
    • Vitengo
      • Huduma za Kisheria
      • Uhasibu na Fedha
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ugavi na Manunuzi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Musoma
    • Wilaya ya Butiama
    • Wilaya ya Bunda
    • Wilaya ya Rorya
    • Wilaya ya Tarime
    • Wilaya ya Serengeti
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Musoma
    • Bunda DC
    • Bunda Mji
    • Butiama DC
    • Rorya DC
    • Tarime DC
    • Tarime Mji
    • Serengeti DC
    • Musoma DC
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • TEHAMA
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu ya Maombi
    • Fomu ya Ahadi ya Uadilifu
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyomba vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio

Mheshimiwa Hapi aanza kukagua miradi ya Halmashauri

Posted on: August 9th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Mara Mheshimiwa Ally Salum Hapi leo tarehe 9 Agosti 2021 ameanza ziara ya kukagua miradi ya maendeleo katika Halmashauri zote tisa za Mkoa wa Mara.

Mheshimiwa Hapi ameanza ziara kwa kutembelea Shule ya Sekondari ya Machochwe iliyopo katika Wilaya ya Serengeti na kuwaagiza Watendaji wa Vijiji na Kata kutoa taarifa za mapato na matumizi kwa wananchi.

“Wananchi hawa wanatakiwa kupata taarifa sahihi za mapato na matumizi kila wakati katika vikao halali na katika mbao za matangazo” alisema Mheshimiwa Hapi.

Aidha Mheshimiwa Hapi ameitaka Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti kukamilisha mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya cha Machochwe kabla ya Desemba, 2021 kuisha.

“Mmeletewa fedha za ujenzi wa kituo cha afya miezi miwili fedha imekaa tu hamjaanza ujenzi na hapa wananchi wanahangaika kutafuta matibabu” alisema Mheshimiwa Hapi.

Mheshimiwa Hapi ametembelea Hospitali ya Wilaya ya Serengeti na kukagua wodi za wagonjwa, nyumba za watumishi na mgahawa vinavyoendelea kujengwa katika hospitali hiyo.

Aidha ametembelea mradi wa stendi ya mabasi ya Mji wa Mgumu  na kuagiza Kamanda wa TAKUKURU Wilaya ya Serengeti kuchunguza mradi wa ujenzi wa stendi hiyo.

“Haiwezekani choo cha matundu 10 na mabafu mawili kinajengwa kwa shilingi milioni 45 ambayo ni sawa na wastani wa shilingi milioni 3,300,000 kwa kila tundu la choo, hii haikubaliki” alisema Mheshimiwa Hapi.  

Mheshimiwa Hapi ameeleza kuwa hajaridhishwa na mradi huo kwani ni fedha nyingi zimetumika lakini majengo ni ya kawaida tu ila gharama zilizotumika ni kubwa.

Mheshimiwa Hapi ametembelea eneo la mradi wa Uwanja wa Ndege wa Mugumu na kumwagiza Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Dkt. Vincent Mashinji kukamilisha mchakato wa ndani na kukamilisha ndani ya mwezi mmoja ili mazungumzo ngazi nyingine yaweze kuanza.

Mkuu wa Mkoa pia ametembelea Shule ya Msingi Mapinduzi B na kukagua mradi wa ujenzi wa madarasa mawili na kuahidi kupeleka mifuko 20 ya sementi kwa ajili ya kukamilisha darasa moja lililojengwa kwa nguvu za wananchi.  

Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa amehitimisha ziara yake kwa kuzungumza na wananchi wa Mji wa Mgumu katika uwanja wa Right to Play ambapo alitumia muda mwingi kusikiliza na kutatua kero za wananchi.

Katika ziara hiyo Mheshimiwa Hapi ameambatana na Mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Serengeti, Mbunge wa Serengeti, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti, watumishi na viongozi wa wilaya, tarafa na kata.

Kesho ziara ya Mkuu wa Mkoa inategemea kuendelea katika Wilaya ya Serengeti ambapo atatembelea kata za Natta, Manchira, Ikoma na Stendi Kuu kukagua miradi ya maendeleo na kuweka mawe ya msingi katika baadhi ya miradi.

Matangazo ya Kawaida

  • WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021 MKOA WA MARA December 18, 2020
  • NAFASI ZA KAZI KWA WALIMU WA MASOMO YA SAYANSI, HISABATI, FUNDI SANIFU MAABARA NA LUGHA June 21, 2018
  • Mara yapaa Kimichezo July 20, 2019
  • JINSI YA KUPATA SALARY SLIP April 23, 2018
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Uthamini wa eneo la Nyatwali umefikia zaidi ya asilimia 50

    January 26, 2023
  • Biashara United yakabidhiwa kwa Mwekezaji

    January 13, 2023
  • Mara yapokea miradi ya zaidi ya milioni 200

    January 13, 2023
  • RC aagiza kukamatwa kwa wazazi ambao hawajapeleka watoto shule

    January 13, 2023
  • Tazama Zote

Video

UMUHIMU WA KULIPA KODI
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Huduma za Maji
  • Mpango wa Manunuzi wa mwaka wa fedha 2017/2018
  • FOMU ZA KUSAFIRI NJE YA NCHI
  • TAARIFA KWA MAKAMU WA RAIS
  • TAARIFA YA HOSPITALI YA WILAYA YA SERINGETI
  • Muongozo wa Matumizi bora ya vifaa vya TEHAMA
  • Maadhimisho ya Kitaifa ya Siku ya Mazingira duniani Mkoani Mara.
  • Zoezi la Unyunyiziaji Kiuatilifu cha Ukoko Majumbani
  • Taarifa kwa Umma-Ziara ya Makamu wa Rais Mkoa wa Mara

Tovuti Mashuhuri

  • IKULU
  • Ofisi ya Rais-TAMISEMI
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifu
  • Ofisi ya Rais-UTUMISHI
  • Idara ya Habari Maelezo

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Katibu Tawala Mkoa wa Mara

    Anwani ya Posta: P.o.Box 299 Musoma

    Simu: +255282622305

    Simu:

    Barua pepe: ras.mara@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti

Hatimiliki©2017 Mkoa wa Mara.Haki Zote Zimehifadhiwa